• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Baraza la Madiwani lapongeza Utendaji kazi wa Rais

Imewekwa: September 10th, 2022

Na Stephen Jackson, Kongwa.

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa,  limempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Halmashauri hiyo fedha kwaajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali.

Pongezi hizo kwa Mhe. Rais, zimetolewa katika baraza la Madiwani lililoketi kujadili taarifa za robo ya nne ya mwaka wa fedha 2021/2022, Septemba 9, 2022.

Akitoa hotuba mbele ya baraza hilo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Mhe. White Zuberi Mwanzalila, amemshukuru Mhe. Rais kwa uongozi wake imara na kuongeza kuwa licha ya changamoto zinazolikabili taifa, lakini usalama pamoja na majukumu ya kitaifa, vimeendelea kuimarishwa.

"Kazi ya Urais siyo kazi ndogo, ndiyo kazi ya mwisho ya uongozi katika Nchi. Anaongoza watanzania zaidi ya milioni sitini. Lakini pamoja na changamoto zote za nchi, bado nchi inaendelea kutekeleza majukumu yake kama kawaida" Alisema Mwanzalila.

Aidha Mhe. Mwanzalila ametumia fursa hiyo kuwasihi watanzania kuendelea kuchangia maendeleo kupitia tozo za miamala kwa kuwa fedha hizo zinatumika kwenye ujenzi wa miradi, na hivyo amewataka Madiwani kuhakikisha wanawaeleza wananchi kuhusu faida za tozo.

" Ni kweli ni ngumu Sana kujichangisha, wengi tunapenda tupewe, tutapewa mpaka lini? ni lazima na sisi kama watanzania tuchangie Maendeleo yetu" Alinukuliwa Mhe. Mwanzalila.

Kwa upande mwingine, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Richard Mwite, ameiomba Serikali kuendelea kuipatia Halmashauri fedha za tozo  kwa mara nyingine kwa kuwa inao uwezo wa kuzisimamia, ikizingatiwa kuwa hali ya makusanyo kwa kipindi cha robo ya nne, Halmashauri ilivuka lengo.

"Kwa taarifa za robo hii tumefanya vizuri katika makusanyo, wala hatuna hoja yoyote. Na niseme tu Mhe. Mwenyekiti, kwa ukaguzi uliopita, Halmashauri yetu imepata hati safi" Alisema Mhe. Mwite.

Sanjali na  hayo yote,  amewaasa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya virusi vya  UKIMWI kwa kuwa ugonjwa huo bado ni tishio.

Amebainisha kuwa kwa kipindi cha Aprili - Juni, 2022,  kati ya watu 4693 waliopimwa kwa hiari,  79 walikutwa na maambukizi ya VVU ambao ni sawa na 4.2%.

Mhe. Mwite ametumia pia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi kuendelea kujitokeza  kupata chanjo ya UVIKO 19, kwa kuwa chanjo hiyo ni muhimu kwa Afya za wananchi.

Kuhusu sakata la utoro shuleni,  Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa, Dkt. Omary Nkullo ameliambia baraza kuwa, imeanzishwa Oparesheni Maalumu ya futa utoro ambapo kwa kushirikiana na jeshi la polisi uongozi utapita katika maeneo mbalimbali kuwakamata wazazi walioshindikana na kuwafungulia kesi.

" Tumekubaliana Jana kwamba wale ambao itashindikana kabisa basi OCD tutakuomba nguvu yako, tutakuwekea mafuta kwenye gari yako, tuzunguke Kijiji kimoja baada ya kingine tukamate wale wazazi ambao walishindikana". Alisema Dkt. Nkullo.

Wilaya ya Kongwa ni miongoni mwa Halmashauri zilizonufaika na miradi iliyotokana na fedha za tozo.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa Kazini September 30, 2023
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA November 02, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba, 2023 November 23, 2023
  • Fomu ya Maelekezo ya kujiunga na shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa. May 18, 2022
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • Elimu ya Rushwa yawakuna Wauguzi, matabibu waiomba TAKUKURU kuwatembelea mara kwa mara.

    November 24, 2023
  • Kamati ya Fedha yasisitiza matumizi mazuri ya fedha

    November 23, 2023
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Dodoma, yapongeza Utekelezaji wa Miradi.

    November 14, 2023
  • Utitiri wa vyombo vya watumia maji, Watajwa kuzorotesha jitihada za Serikali huduma bora za maji vijijini

    November 03, 2023
  • Tazama Yote

Video

Viongozi Kongwa Wajivunia hati safi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)
  • Bunge la Tanzania

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.