JAMII YATAKIWA KUSHIRIKI KUTANGAZA KWA KUTUMIA BIDHAA ZINAZOZALISHWA VETA
Na Bernadetha Mwakilabi
Habari – Kongwa DC
Wananchi wametakiwa kushiriki katika kutangaza kwa kutumia bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na wanafunzi wa chuo cha ufundi stadi VETA kwa kuzitumia ili waweza kuwaunga mkono na kuthamini mafunzo hayo.
Hayo yameelezwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Ndg. Fortunatus Mabula alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya tatu ya wahitimu 80 wa ngazi ya pili katika fani mbalimbali katika chuo cha ufundi stadi VETA Kongwa ambapo ameeleza kuwa chuo hicho kipo kwa ajili ya kusaidia jamii moja kwa moja hivyo jamii itumie bidhaa kama matofari, huduma ya matengenezo ya magari na ushonaji nguo zinazozalishwa na wanafunzi hao ili kuwaunga mkono.
Katika mahafali hayo Mgeni Rasmi alipata wasaa wa kutembelea karakana za ushonaji, magari, umeme na kiwanda cha kufyatua matofali ambapo alisistiza uongozi wa chuo cha VETA Kongwa kutangaza kazi wanazozifanya ili jamii iweze kuwaunga mkono kwa kutumia bidhaa zao
Licha ya Ndg. Mabula kuwasihi wazazi kutumia chuo cha VETA kuwapeleka watoto kupata ujuzi na kuepuka kukaa nyumbani na Watoto wasiokuwa na shughuli za kufanya lakini pia amewasihi wahitimu wazingatie maadili na kutumia vema ujuzi walioupata ili kuwainua kichumi na kusaidia Taifa kwa ujumla kwani elimu ya VETA ni ujasiriamali wa moja kwa moja.
Akiongea wakati wa hafla za mahafali hayo Kaimu Mkuu wa chuo cha VETA Kongwa Ndg. John Magulyati ameleza kuwa ili kuhakikisha hakuna mtanzania anayekosa elimu kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo wanafunzi waliokatisha masomo kutokana na kupata ujauzito, chuo kimeanza kutoa kozi za muda mfupi kwa mabinti wanaonyesha watoto wenye umri kuanzia miezi mitatu.
Katika Risala yao wahitimu hao wameomba Serikali kuwasaidia kwa kuwawezesha vitendea kazi katika fani zao pindi wanapohitimu mafunzo yao ili iwe rahisi kwao kujiajiri na kufanya ujasiriamali.
Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya
Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma
Simu ya Mezani: +255 26 2370031
Simu ya Mkononi: +255 713399349
Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz
Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.