• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

"Posho, Maslahi Binafsi Visiwe Kipaumbele kwenye Miradi ya Maendeleo"" DC Mwema.

Imewekwa: October 16th, 2023

Na Stephen Jackson, Kongwa DC

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma Mhe. Remidius Mwema Emmanuel amewataka wasimamizi wa miradi mbalimbali ya kijamii inayotumia fedha za  umma kuandaa bajeti zenye tija Ili kuyafikia malengo ya miradi hiyo badala ya kuweka vipaumbele kwenye malipo ya posho na maslahi binafsi.

Mhe. Mwema amesema hayo wakati wa kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi (PHC) kilichofanyika Oktoba 13, 2023 katika ukumbi wa Hospitali ya Wilaya ya Kongwa.

Akiwasilisha mada katika kikao hicho kuhusu mradi wa Uendelevu wa Maji na Usafi wa Mazingira "P4R" Afisa Afya Wilaya bwana Abdulrahman Shehe Othman ametaja malengo ya mradi huo kuwa ni pamoja na kuboresha miundombinu ya Maji na Usafi wa Mazingira katika Vituo vya kutolea Huduma za Afya katika Halmashauri, Kuhamasisha ujenzi na matumizi ya vyoo bora katika ngazi ya kaya pamoja na kuhimiza tabia ya kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni.

Programu ya "P4R" inatekelezwa Kwa ushirikiano wa Benki ya Dunia na Serikali ya Tanzania kupitia "force Account" katika Halmashauri 137 ndani ya mikoa 25 ya Tanzania kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka wa fedha 2023/2024, Mkoa wa Dodoma na Halmashauri 6 zikiwa ni miongoni mwa wanufaika katika awamu ya pili ambapo jumla ya Shilingi 238,848,519.12 zimepokelewa katika maeneo ya utekelezaji Wilayani Kongwa.

Programu hiyo inatekelezwa katika zahanati tatu za Manyata, Hembahemba na Msunjilile ambazo zimetengewa jumla ya shilingi 160,723,614.00 huku  CHMT ikitengewa Shilingi 78,124,905.12

Wa pili kulia ni Afisa Afya (W) Abdulrahman Shehe Othman akisikipokea michango ya mawazo mara baada ya kuwasilisha mada. Picha na Stephen Jackson.

Naye Mratibu wa Chanjo na mnyororo baridi Kongwa (DIVO) Bwana Cosmas Mlimila aliwasilisha mada kuhusu Tahadhari ya Mlipuko wa ugonjwa wa Surua, na kwamba huduma ya chanjo  kwa watoto wote ambao hawakukamilisha au kutochanja kabisa inatarajiwa kutolewa Kwa misingi ya dharula.

Mlimila amezitaja dalili za ugonjwa wa Surua kuwa ni pamoja na Homa kali, Vipele, Macho kuwa mekundu, Kikohozi na Mafua Huku athari zake zikiwa ni Nimonia kali Upofu wa Macho, Homa ya uti wa mgongo na hatimaye Kifo. Aidha alifafanya kuwa ugonjwa wa Surua husambazwa kwa njia ya Kikohozi au chafya kutoka kwa mtu aliyeambukizwa na dalili zake huweza kuonekana kuanzia siku 7 hadi 18.

Miongoni mwa Mikakati ya kukabiliana na Ugonjwa wa Surua Wilayani Kongwa ni pamoja na kuwatafuta watoto wote ambao hawajakamilisha chanjo au kutochanja kabisa, utoaji wa Elimu Kwa Jamii na kuhakikisha upatikanaji wa chanjo na kuimarisha huduma za mkoba.

Katikati ni Bwana Cosmas Mlimila, Mratibu wa Chanjo na mnyororo baridi (DIVO) akifuatilia mjadala baada ya kuwasilisha mada ya tahadhari ya mlipuko wa Surua.

Mhe. mwema alihitimisha kikao hicho kwa kusisitiza mapitio ya bajeti katika mradi wa "P4R" Ili kuhakikisha tija inakuwepo Kwa kuleta Matokeo chanya huku Suala la tahadhari ya mlipuko wa Surua likisimamiwa kikamilifu.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.