WALIOVAMIA MAENEO YA UWANJA WA NDEGE WARIDHIA UTARATIBU MPYA
Na Bernadetha Mwakilabi
Habari - Kongwa DC
Wakulima wanaofanya shughuli zao za kilimo katika maeneo ya uwanja wa ndege Kongwa wamekubaliana na maelekezo yaliyotolewa na mkuu wa wilaya ya kongwa mhe. Mayeka Simon Mayeka pamoja na uongozi wa mamlaka ya viwanja vya ndege Mkoa wa Dodoma juu ya utaratibu mpya wa matumizi ya maeneo hayo.
Wakiongea mbele ya Mhe. Mkuu wa Wilaya wakulima hao kwanza wamekiri kuvamia maeneo hayo miaka mingi iliyopita na kwamba wamekuwa wakitumia maeneo hayo kinyume cha utaratibu hivyo wapo tayari kufuata utaratibu mpya wa kutumia maeneo hayo kihalali na pindi Serikali itakapohitaji kufanya mwendelezo wa uwanja huo watakuwa tayari kuachia maeneo hayo.
Awali katika mkutano huo Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka amesema uwanja huo haukufungwa bali ulipunguza matumizi hivyo utarejeshwa wakati wowote kwa ajili ya matumizi hivyo wakulima wataanza kulima kwa kukodi maeneo hayo kwa gharama za shilingi 15,000 kwa hekari moja hadi pale watakapopatiwa taarifa za usitishaji wa shughuli zao.
Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya
Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma
Simu ya Mezani: +255 26 2370031
Simu ya Mkononi: +255 713399349
Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz
Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.