WATANO WASIMAMISHWA KAZI MAMLAKA YA MJI MDOGO KIBAIGWA
Na Bernadetha Mwakilabi
Habari kongwa DC
Viongozi watano wa Mamlaka ya Mji mdogo Kibaigwa Wilayani Kongwa wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi kutokana na tuhuma za kuuza maeneo ya ardhi yaliyotengwa kwa ajili ya malisho katika eneo la Ndurugumi na kusababisha migogoro baina ya wakulima na wafugaji.
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka Simon Mayeka amewasimamisha kazi viongozi hao alipofika katika Mamlaka ya Mji mdogo Kibaigwa kusuruhisha mgogoro wa ardhi uliopo baina ya wakulima na wafugaji ambapo wakulima walivamia eneo lililotengwa kwa ajili ya malisho na wafugaji kuweka makazi katika hilo.
“nataka kujua hekari 600 za kilimo ziko wapi, hekari 2000 za malisho ziko wapi na kwanini eneo la malisho kuna makazi nae neo la kilimo kuna visima vyenye mkataba wa kutumia kwa mwaka mmoja mmoja” alisema Mayeka.
Akiongea katika mkutano huo Mhe. Mayeka amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa kwa kushirikiana na Idara ya Ardhi kurudi kuja kupima upya eneo la wafuaji na wakulima kuweka vitalu ili wafanye shughuli zao kwa utaratibu.
Aidha mhe. Mayeka ameelekeza kuwa anatoa muda wa siku 90 kwa wafugaji wote walioweka makazi katika eneo la malisho wawe wameondoka katika maeneo hayo.
Akiongea katika mkutano huo Afisa Mipango Miji Wilaya ya Kongwa Bw. Meshack Mlaponi ameeleza kuwa mgogoro huo wa kuvamia maeneo ya kilimo na malisho upo tangu mwaka 2007 kibaigwa ilipopewa hadhi ya kuwa Mamlaka ya Mji mdogo na Kijiji cha Ndurugumi kuwa sehemu ya kibaigwa ambapo baadhi ya viongozi wanatajwa kushiriki kwa kutoa nyaraka za kufoji kuwapatia Wananchi maeneo hayo.
Hata hivyo nae diwani wa Kata ya Kibaigwa Mhe. Daudi Kweka ameweka wazi viongozi kutokuwa na usimamizi mzuri wa mipaka ya ardhi iliyowekwa hali iliyopepelekea migogoro hiyo hivyo ameahidi kujipanga upya kurekebisha makosa yote yaliyofanyika hapo awali.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kitongoji cha Sabasaba anaeleza kuwa viongozi waliruhusu wafugaji kulisha mifugo na sio kuweka makazi lakini baada ya kutokea mafuriko waliwaruhusu kuhamia katika eneo la malisho na kuishi muda lakini baada ya hapo baadhi yao hawakurudi.
Kwa upande wao wananchi wa mamlaka ya mji mdogo Kibaigwa wakiongea mbele ya Mkuu wa Wilya ya Kongwa katika mkutano huo wameiomba Serikali kuwahamisha mara kwa mara viongozi wanaofanya kazi na Wananchi kwani kuna wakati viongozi wanaishi muda mrefu katika eneo moja wanajenga mazoea na wananchi hadi wanasahau kutimiza wajibu wao.
Viongozi hao waliosimamishwa kazi ni Mtendaji wa Mamlaka (TEO) Bi. Foska Mgovano, Mtendaji Kata Kibaigwa Bw. Venant Tibandolage, Mwenyekiti wa Mamlaka Ndg. Nicolus Iyanex, Mwenyekiti wa Kitongoji cha Karume Ndg. Stanley Myoka na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Sabasaba Ndg. Kedmon Mbaluka ambapo wamesimamishwa kazi kwa muda wa siku 90 baada ya tume iliyoundwa kukamilisha uchunguzi wake.
Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya
Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma
Simu ya Mezani: +255 26 2370031
Simu ya Mkononi: +255 713399349
Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz
Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.