• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Waziri Mkuu Azitaka Halmashauri Zote Nchini Kusimamia Ukusanyaji wa Mapato

Imewekwa: October 28th, 2018

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kasimu Majaliwa (MB) ametoa rai kwa Madiwani, Wakurugenzi na Makatibu Tawala wa Mikoa  kubadilisha mtazamo  katika suala zima  la usimamizi, ukusanyaji na  utumiaji  wa fedha  zinazokusanywa kwenye Halmashauri zote nchini

Akifungua Mkutano Mkuu wa 34 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) uliofanyika leo katika ukumbi wa Jakaya Mrisho Kikwete Jijini Dodoma. Mhe. Majaliwa amesema ustawi wa jamii unategemea uwezo wa mapato yake na matumizi yenye tija kwa fedha zinazokusanywa

Mhe. Majaliwa amefafanua kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha Halmashauri zinakuwa na uwezo wa kujitegemea kimapato kwa zaidi ya asilimia 80 ifikapo mwaka 2025 ili kutimiza lengo la Serikali katika Dira ya Maendeleo ya 2025.

Amesema kuwa Serikali ya awamu ya Tano imekuwa ikichukua  hatua mbalimbali  ili kuhakikisha dira ya maendeleo ya mwaka 2025 kwa kuanzisha  utaratibu wa kugharamia  miradi  ya kimkakati  yenye lengo  la kuziongezea Halmashauri mapato  ya uhakika  na kupunguza utegemezi  wa ruzuku  ya Serikali.

Mhe. Majaliwa amesema kuwa  hadi sasa Serikali  imeidhinisha shilingi bilioni 131.5 kutekeleza miradi ya  ipatayo 22 katika Halmashauri  17 zilizokidhi vigezo kwenye Mikoa 10 na mpaka sasa kiasi cha shilingi bilioni 16.4 zimepelekwa kwenye Halmasahauri  hizo kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa  miradi ya kimkakati.

Amaesema kuwa  uchambuzi wa miradi  mingine ya kimaendeleo  unaendelea na Halmashauri  zitakazokidhi vigezo zitapata fedha kwa  ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo na amezitaka Halmashauri zote nchini  kutumia fedha  hizo kwa ajili ya  malengo yaliyokusudiwa.

“ Serikali  haitakuwa  na utaratibu wa kutoa fedha bila kufahamu kwa kina fedha hizo zinakwenda kufanya nini na zinaleta mabadiliko gani kwa kuwa nimesikia kwamba katika baadhi ya Halmashauri fedha zilizokwishatolewa bado hazijaanza kutumika kikamilifu, nawaagiza Waheshimiwa Madiwani kusimamia matumizi ya fedha hizo ili Halmashauri  zipate miradi yenye ubora unaotakiwa na inayokamilika kwa wakati” Anafafanua Majaliwa.

Mhe. Majaliwa amesema Serikali imeongeza ukusanyaji wa mapato  katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kuhakikisha Halmashauri zote 185 zinatumia Mfumo wa ukusanyaji wa mapato wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na kufanya ongezeko la mapato kutoka shilingi bilioni 379 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia  shilingi bilioni 553.39 kwa mwaka wa fedha 2017/2018 .

Amewaonya Viongozi wa Halmashauri wanaolalamikia kutokuendelea kulalamika  kuhusu baadhi ya vyanzo  vya mapato  kuchukuliwa na Serikli  kuu bali  waongeze  bidii  na ubunifu  katika kutafuta  vyanzo vipya vya  mapato ili Mamlaka za Serikali za Mitaa  ziweze kujitegemea.

“Fanyeni kazi  ionekane, tusione Mamlaka  za Serikali za Mitaa ambazo kweli zinatoa huduma, tuone vyumba vya madarasa vinaongezeka, watoto hawakai chini, Zahanati zinazopendeza  hapo tunaweza  kusema sasa  Halmashauri zimekomaa” Amefafanua Mhe. Majaliwa

 Wakati huo huo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Mhe. Selemani Jafo amewaagiza Wakurungenzi wa Halmashauri kuacha kufanyakazi kwa mazoea bali wafanye kazi kwa bidii kwa kutumia weledi ili  kuleta mabadiliko katika utendaji kazi katika Halmashauri

Aidha Mhe. Jafo amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanatenga fedha kwa ajili ya kuwakopesha wanawake, vijana  na watu wenye ulemavu ili kuwawezesha kiuchumi  na kupunguza umaskini  nchini.

Mkutano huu umehudhuriwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Mhe. White Zuberi Mwanzalila ambaye pia Mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Dodoma pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kongwa Dkt. Omary A. Nkullo.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.