• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Kampeni ya kuhamasisha Usajili na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto chini ya miaka mitano wilayani Kongwa yazinduliwa

Imewekwa: June 28th, 2021

Na Stephen Jackson - Kongwa

 

Mkuu wa wilaya ya Kongwa Mhe. Remedius Mwema Emmanuel, amezindua kampeni ya siku tano ya kuhamasisha zoezi la usajili na utoaji vyeti vya kuzaliwa kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano.

Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo ambao ni Maafisa watendaji wa Kata, vijiji, na watumishi wa Afya kutoka vituo vya Afya na zahanati mbalimbali wilayani hapa, Mhe. Mwema ameonesha kuthamini ushiriki wa kila mmoja katika mafunzo hayo na hivyo amewaagiza kufanya kazi kwa weledi na uadilifu.

Wakati huo huo ameonya tabia ya baadhi ya watu wasio waaminifu wanaoweza kutumia zoezi la utoaji vyeti, kama sehemu ya kujinufaisha kwani kufanya hivyo ni kuichafua serikali na viongozi wake.

Katika hatua nyingine amewaagiza Maafisa watendaji wa kata kuhakikisha fomu mbalimbali zinazohusiana na masuala ya huduma za serikali zinapatikana katika ofisi za kata ili kupunguza usumbufu kwa wananchi kusafiri umbali mrefu.

Kuhusu utoaji vyeti bure amefafanua kuwa thamani ya vyeti hivyo iko palepale isipokuwa serikali na wadau wengine wanalipia gharama badala ya mwananchi.

Ametumia pia fursa hiyo kuipongeza mamlaka ya usajiri wa vizazi na vifo (RITA) kwa kufanya maboresho chanya, na hivyo kuwataka wadau wa zoezi hilo kuunga mkono juhudi hizo kwa kufanya kazi kwa bidii na uadilifu ili wilaya ya Kongwa iweze kuibuka kinara kwa kufanikisha zoezi hilo kikamilifu. ‘’Natamani katika Halmashauri nyingine zikienda kusimama na kuzungumza zitolee mfano wa Kongwa kwa kufanikisha jambo hili kwa ufanisi mkubwa sana’’.

Kwa upande wa washiriki wa mafunzo hayo wamemhakikishia Mkuu wa wilaya kuwa watafanya kazi kwa ufanisi mkubwa kwa kuwatawapatia vyeti watoto wote walio chini ya miaka mitano kwa kuzingatia utaratibu uliotolewa kama juhudi mojawapo za kufikia lengo lililowekwa kiwilaya la kusajili watoto elfu nane (8,000).

Kampeni na mafunzo ya usajili na utoaji vyeti kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano, yameratibiwa na Idara ya Maendeleo ya Jamii na kusimamiwa na Mratibu wa RITA wa Halmashauri ya Kongwa Bi. Yovina Richard Mauki, ambapo Mafunzo yametolewa na Bwana Adam Phidel Nkolabigawa ambaye ni Msajili wa vizazi na vifo kutoka Makao makuu ya RITA - Ofisi kuu ya Dodoma.

Akitilia mkazo mambo ya kuzingatia, bwana Nkolabigawa amewaagiza wasajili wasaidizi kutosajili wateja wasio na kielelezo chochote, kutotumia vibaya laini za simu zinazotumika kwenye usajili, na pia kuepuka kufuta vyeti vya kuzaliwa, kwa kuwa kitendo hicho hakiruhusiwi.

 

Kufuatia mafunzo hayo baadhi ya washiriki wametoa maoni yao kuhusu namna ya kuboresha huduma ya usajili wa watoto pindi wanapozaliwa, kwani kumekuwa na changamoto kwa baadhi ya wazazi kutowapa majina kwa wakati watoto wao jambo linalochelewesha usajili.

Bibi Zainabu Kudomu, ambaye ni Muuguzi katika Kituo cha Afya Mlali, amependekeza kuongezwa kwa kipengele katika kadi ya mama mjamzito kitakachompa nafasi mjamzito kupendekeza majina mawili ya mtoto anayetarajiwa kuzaliwa moja likiwakilisha jinsi ya kike na lingine jinsi ya kiume. Akijibu hoja hiyo, mwezeshaji Bwana Adam Phidel Nkolabigawa ameunga mkono hoja hiyo.

Uzinduzi wa kampeni hiyo umefanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari Kongwa, ambapo jumla ya washiriki wapatao 165 wakiwemo watumishi wa Afya, Maafisa watendaji wa kata na vijiji na wawezeshaji kutoka ngazi ya mkoa na wilaya walihudhuria. Kampeni hiyo ya siku tano itaanza kesho siku ya Jumanne tarehe 29/06/2021 katika kata zote za wilaya ya Kongwa.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.