• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

DED KONGWA AZINDUA DARASA JANJA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA KIBAIGWA

Imewekwa: October 9th, 2025

DED KONGWA AZINDUA DARASA JANJA

Na Bernadetha mwakilabi

Habari – Kongwa DC

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Dkt. Omary Nkullo amezindua darasa janja katika shule ya wasichana Kibaigwa litakalowasaidia wanafunzi kusoma Kiteknolojia zaidi.

Baadhi ya miundombinu iliyofungwa katika darasa janja.

Akiongea wakati akizindua darasa hilo Dkt. Nkullo amesema kuwa anategemea mabadiliko makubwa ya kitaaluma katika shule hiyo tofauti na shule zingine Wilayani Kongwa kwani hakuna kisingizio kwa walimu na wanafunzi cha kushindwa kujifunza kutokana na miundombinu ya kisasa iliyowekwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Dkt. Omary Nkulo akivishwa skafu na wanafunzi alipowasili shuleni hapo.

Aidha Dkt. Nkullo licha ya kusisitiza kutunzwa na kulindwa kwa muundombinu huo kwa kuweka kamera za ulinzi lakini pia ameshauri wataalamu wa tehema kuweka program ya Akili Unde ili kusaidia kupata majibu ya maswali yanayowatatiza wanafunzi katika ujifunzaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Dkt. Nkullo akiongea wakati wa akizindua darasa janja.

Kwa upande wake Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Kongwa Mwl. Sudy Abdul amesema kuwa darasa janja hilo lenye smart board lililofadhiliwa na SEQUIP ni la kwanza katika Wilaya ya Kongwa likifuatiwa na darasa la shule ya Sekongari Manungu.

Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Kongwa Mwl. Sudy Abdul akiongea wakati wa uzinduzi.

Vilevile Mwl. Sudy ameongeza kuwa uwepo wa darasa hilo lenye Televisheni za kujifunzia zilizounganishwa na mfumo wa Intaneti utafanya shule ya wasichana Kibaigwa kuwa bora na kisasa zaidi ambapo mwalimu mmoja anaweza kufundisha wanafunzi wa shule nne kwa wakati mmoja na wanafunzi hao wakaonana na kushirikiana kupitia Televisheni hizo.

Akitoa shukrani zake mwalimu mkuu wa shule ya wasichana Kibaigwa Mwl. Gemma Kihwelo ameahidi kuutunza muundombinu huo na kuwasimamia vema walimu na wanafunzi wake kuhakikisha wanajifunza kupata matokeo bora zaidi.

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya wasichana ya Kibaigwa Mwl. Gemma kihwelo akitoa neno la shukrani.

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kazini September 23, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili September 02, 2025
  • Tangazo la nafasi ya kazi June 13, 2025
  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • DED KONGWA AZINDUA DARASA JANJA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA KIBAIGWA

    October 09, 2025
  • TRA KONGWA WAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA

    October 09, 2025
  • DC KONGWA AKAGUA MIRADI YA ELIMU KATA YA LENJULU

    October 08, 2025
  • MAAFISA KILIMO WAMEAGIZWA KUWASAJILI WAKULIMA ILI WAWEZE KUPATA MBEGU ZA RUZUKU

    October 08, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.