• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

DC KONGWA AZINDUA JUKWAA LA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI NGAZI YA WILAYA

Imewekwa: October 24th, 2025

DC KONGWA AZINDUA JUKWAA LA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI NGAZI YA WILAYA

Na Bernadetha Mwakilabi

Habari – Kongwa DC

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka Simon Mayeka amezindua jukwaa la kuwawezesha wanawake kiuchumi ngazi ya Wilaya lenye lengo kubwa la kuleta mapinduzi makubwa ya kimaendeleo kwa wanawake na kuleta ufanisi katika maendeleo.

Akizindua jukwaa hilo mwishoni mwa juma lililopita Mhe. Mayeka ameeleza kuwa kupitia jukwaaa hilo wanawake Wilayani kongwa watapata manufaa makubwa ikiwemo kutafuta masoko ya biashara yatakayowainua kiuchumi na kama watalitumia vizuri jukwaa hilo jamii itashuhudia wanawake watakavyoinuka.

Baadhi ya wanawake wanaounda jukwaa hilo wakati wa uzinduzi uliofanyika ukumbi wa Veta Kongwa

Aidha Mhe. Mayeka amewataka wanawake kuwa na nguvu katika kusimamia jukwaa hilo kwa kutafuta watu wa kuwasaidia kuwashika mkono na kuwainua na kwamba jukwaa hili ni ajenda muhimu itakayowawezesha wanawake kiuchumi ngazi ya familia hadi taifa.

Nae Katibu Tawala Wilaya ya Kongwa Bi. Sozi Ngate amepongeza viongozi waliochaguliwa kuongoza jukwaa hilo na kuwataka kufanya kazi kuhakikisha wanawake wote wanainuka kiuchumi ili kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan ambaye katika awamu yake wanawake wamepata fursa nyingi.

Katibu Tawala Wilaya ya Kongwa Bi. Sozi Ngate akiongea wakati wa uzinduzi wa jukwaa hilo

Akiongea katika uzinduzi huo Ofisa Maendeleo ya Jamii Bi. Faraja Kasuwi ameeleza kuwa wanawake 88 kutoka Kata zote 22 za Wilaya ya Kongwa wanaunda jukwaa hilo na kwamba jukwaa hilo ni muhimu kwa jamii kwani mwanamke akiwezeshwa familia inakuwa imara.

Afisa Maendeleo ya Jamii Bi. Faraja Kasuwi akifafanua lengo la jukwaa hilo

Pamoja na hayo nae Mwenyekiti wa jukwaa hilo ngazi ya Wilaya Bi. Joyce Mahemu kutoka Kata ya Mlali amesema kuwa wakati wa uundwaji wa jukwaa hilo walipata elimu ya fursa mbalimbali zikiwemo kilimo mifugo madini ujenzi biashara elimu ya jamii kama malezi maadili uongozi wa siasa sayansi na teknoloji.

Mwenyekiti wa jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi wilaya ya Kongwa Bi. Joyce Mahemu akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi

Aidha Bi. Mahemu ameahidi kufanya kazi kwa maelekezo waliyopewa na kuhakikisha wanakuwa chachu katika kuhimiza maendeleo kwa wanawake wenzao na jamii kwa ujumla na wapo tayari kupiga Kura ifikapo Oktoba 29 2025.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAFUNZO KWA WASIMAMIZI NA WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI -JIMBO LA KONGWA. October 22, 2025
  • TANGAZO LA MAFUNZO KWA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA - JIMBO LA KONGWA. October 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGA KURA JIMBO LA KONGWA October 14, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini September 23, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • DC KONGWA AZINDUA JUKWAA LA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI NGAZI YA WILAYA

    October 24, 2025
  • KONGWA YATOA ZAIDI YA MILIONI 216 MIKOPO 10% AWAMU YA KWANZA 2025/2026

    October 23, 2025
  • DC KONGWA ASISITIZA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA

    October 14, 2025
  • DED KONGWA AZINDUA DARASA JANJA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA KIBAIGWA

    October 09, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.