• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

ALAT DODOMA YAPONGEZA UFANISI MIRADI KONGWA

Imewekwa: May 25th, 2024

Na Stephen Jackson, Kongwa DC

Wajumbe wa ALAT Mkoa wa Dodoma chini ya Mwenyekiti wake Mhe. White Zuberi Mwanzalila Mwenyekiti wa Halmashauri na Diwani wa Kata ya Kongwa, na Katibu wake Bi. Mwanahamis Ally Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa, wamepongeza viwango vya utekelezaji miradi katika Halmashauri ya Kongwa.

Pongezi hizo zimetolewa 25 Mei, 2024, na wajumbe wa mkutano wa ALAT utakaofanyika siku ya Jumapili 26 Mei, 2024 Mjini Kongwa. wakati wa ziara ya Ukaguzi wa miradi inayotekelezwa Wilayani Kongwa.

Baadhi ya wajumbe wa ALAT wakiwa ndani ya Jengo la maabara shule ya Sekondari Laikala wakati wa ziara ya Ukaguzi.

Akishauri kuhusu kasi ya mradi wa Jengo la Halmashauri linalojengwa na Mkandarasi SUMA - JKT, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Mhe. Donald Mejeti, alishauri mkandarasi kuongeza kasi ya ujenzi ili kuharakisha ukamilishaji wa jengo hilo lenye ghorofa moja.

Wajumbe wa ALAT wakikagua Jengo jipya la Halmashauri wakati wa ziara ya ukaguzi miradi.

Wakikagua miradi mbalimbali baadhi ya wajumbe wameahidi kupanga muda zaidi wa kufika kujifunza mbinu na mikakati ambayo Halmashauri ya Kongwa imekuwa ikitumia kukamilisha miradi kwa bajeti zilizopangwa, huku sehemu ya fedha ikisalia na kutumiwa kwa ajili ya maboresho miundombinu mingine.

Sehemu ya ndani ya Jengo la Maabara jumuishi (Multipurpose) shule ya Sekondari Laikala iliyojengwa kwa mapato ya ndani ya Halmashauri.

Akipongeza mradi wa Jengo la maabara shule ya Sekondari Laikala, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mpwapwa Mhe. George Fuime aliwataka viongozi kushirikiana na Wananchi kuhakikisha watoto wao wanatumia Miundombinu inayojengwa kujipatia Elimu badala ya kukimbilia mijini kufanya shughuli za ndani.

Diwani wa Kata ya Lenjulu Mhe. Brighton Chisongela ameshukuru ujio wa ALAT Mkoa katika Kata hiyo licha ya Halmashauri kuwa na Kata nyingi, kubwa zaidi akiishukuru Halmashauri ilivyoweza kutoa fedha za mapato ya ndani kujenga Kituo hicho cha Afya ambacho kimeendelea kuboreshwa kwa  kujengewa Miundombinu mbalimbali ikiwemo Jengo la maabara.

Diwani Kata ya Lenjulu Mhe. Brighton Chisongela akifurahia jambo pamoja na wajumbe wengine.

Nao baadhi ya Wananchi walipofika Kwenye Kituo hicho cha Afya licha ya kupongeza jitihada za Serikali, pia wameiomba Serikali kuleta wataalamu wa Afya katika Kituo hicho ambacho kwa Sasa kina wataalamu wawili tu, jambo ambalo Mkurugenzi Mtendaji Kongwa Dkt. Omary Nkullo ameahidi kulifanyia kazi kikamilifu.

Miradi iliyokaguliwa na ALAT ni Jengo la Utawala la Halmashauri linalojengwa kwa fedha kutoka Serikali kuu, kikundi cha Wanawake cha Ushonaji nguo Kongwa Mjini, Mradi wa Maji Kijiji cha Laikala "B" unaotekelezwa na RUWASA,  Maabara jumuishi (Multipurpose ) Shule ya Sekondari Laikala iliyojengwa kwa Mapato ya ndani, na Jengo la maabara ya Kituo cha Afya Lenjulu ambalo pia limejengwa kwa fedha za Makusanyo ya ndani ya Halmashauri.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.