• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Baraza la Biashara Lajadili Masuala Yanayokwaza Uwekezaji na Ukuaji wa Biashara Wilayani Kongwa

Imewekwa: September 17th, 2018

Baraza la Biashara la Wilaya ya Kongwa limefanya kikao maalum kuhusu kuweka mazingira bora na rafiki ya kukuza biashara zilizopo pamoja na kuibua biashara mpya wilayani humo.

Mchokoza mada kutoka shirika la uboreshaji wa Mazingira ya Biashara ya Ndani (Local Investment Climate - LIC) Ndugu Donald Liya ameeleza kwamba baada ya Serikali kuhamishia Makao Makuu yake katika Jiji la Dodoma, Mkoa wa Dodoma umekuwa na fursa nyingi za uwekezaji na wadau wengi wamekuwa wakifika katika Ofisi ya LIC Jijini Dodoma kutafuta fursa za uwekezaji.  Hivyo, kama Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa haijajiandaa vema itapoteza fursa hii ya Dodoma kuwa Makao makuu ya nchi.

 Aidha, amefafanua sehemu zenye mapungufu katika Halmashauri ya Kongwa kuhusiana na masuala ya uendelezaji na uibuaji wa biashara kwa mujibu wa tafiti ndogo iliyofanyiwa na LIC, ambapo amezitaja changamoto hizo ni; huduma kwa wateja (wafanyabiashara au wawekezaji) ikiwemo utoaji wa taarifa sahihi kwa wakati; upatikanaji wa umeme wa uhakika; upatikanaji usioridhisha wa huduma za maji kwa ajili ya matumizi mbalimbali; upatikanaji wa ardhi iliyopimwa kwa ajili ya uwekezaji na biashara;  kukosekana kwa taasisi muhimu zinazochochea biashara na uwekezaji kama vyuo, taasisi za fedha (banks), shule nzuri binafsi, kampuni za afya, maeneo ya michezo na burudani,  n.k.; utitiri wa tozo kwa biashara – tozo ngazi ya Halmashauri na Serikali Kuu; miundombinu duni hasa kutoka maeneo ya uzalishaji.

Baada ya mchokoza mada kuwasilisha mada, Wajumbe walijadili changamoto zilizobainshwa na kisha kufikia maazimio yafuatayo;

  1. Kila Taasisi za Umma itoe elimu kwa watumishi wake juu ya huduma kwa wateja;
  2. Viongozi wasimamie wataalam na wafanyabiashara kuhakikisha wanatoa huduma nzuri kwa wateja;
  3. Huduma kwa Wateja iwe agenda ya kudumu na kuwekewa mikakati;
  4. Kila Ofisi iweke bango litakaloonesha mawasiliano ya Mkuu wa Taasisi kusaidia wateja waliopata huduma isiyo rafiki;
  5. Wizara ya Elimu iingize Huduma kwa Mteja kuwa sehemu ya mtaala wa elimu;
  6. Ofisi ya Mkuu wa Wilaya iunde timu itayounganisha taasisi wezeshi kutatua changamoto mbalimbali katika maeneo ya kimkakati – upimaji wa viwanja na uwekaji wa miundombinu wezeshi kuvutia uendelezaji wa viwanja katika maeneo hayo;
  7. Ofisi ya Mkuu wa Wilaya iunde Kamati itakayoonesha na kuongoza njia ya uwekezaji. Aidha, Kamati hiyo iainishe vipaombele vya uwekezaji ndani ya Wilaya;
  8. Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ifupishe muda wa ufungaji wa umeme kwa wateja;
  9. Gharama ya Umiliki ardhi kwa mwekezaji iwe rafiki ili kumvutia awekeze; aidha, Halmashauri ifanye huduma na siyo ifanye biashara;
  10. Ushirikishaji kwa wafanyabiashara ufanyike wakati Halmashauri inapopanga tozo;
  11. Ofisi ya mkuu wa wilaya iunde timu ndogo ambayo itatathimini na kuainisha tozo ziwe rafiki na kulipa;
  12. Halmashauri kufuatilia na kutoa msukumo kwa Taasisi ambazo zimeonesha nia ya kuwekeza ndani ya Wilaya mfano VETA na Wizara ya Maji katika ujenzi wa vyuo;
  13. Halmashauri iandae timu itakayokuwa ikiandika maandiko ya miradi ya kimkakati ndani ya wilaya;
  14. TARURA Wilaya ya Kongwa iweke kanzidata ya Wilaya kwenye miundombinu na kuweka vipaombele;
  15. Elimu ya uanzishaji wa biashara itolewe kwa wote kati ya Mamlaka ya Mapato (TRA) na  Ofisi ya Biashara ya Wilaya;
  16. TRA, Ofisi ya Afya, Ofisi ya Biashara zishirikiane kwa pamoja kuunda Jarida/Kipeperushi kitakachoonesha mwongozo wa uanzishaji wa biashara.

Kikao hiki cha Baraza la Biashara la Wilaya maalum kimefanyika Septemba 12, 2018 ambapo mbali na wajumbe wake limehudhuriwa na wageni walikuwa wakiwemo Wakuu wa Taasisi mbalimbali Wilayani Kongwa, Waheshimiwa Madiwani – Wakuu wa Kamati za Kudumu, na wageni toka Mkoani.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.