• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

BARAZA LA MADIWANI LAJA NA SULUHU FIDIA ZA MAENEO YA JESHI.

Imewekwa: October 31st, 2024

Mkutano wa Baraza la Madiwani Kupokea na Kuidhinisha taarifa za Kamati za kudumu ikiwemo Kamati ya Kudhibiti Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI, Kamati ya Huduma za Jamii, Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira, Kamati ya Maadili, Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango, taarifa ya Mamlaka ya Mji Mdogo wa Kongwa, taarifa ya Mamlaka ya Mji Mdogo wa Kibaigwa kwa kipindi cha robo ya Kwanza (Julai - Septemba, 2024) kwa mwaka wa fedha 2024/2025 umefanyika tarehe 31 Oktoba 2024.

Katika mkutano huo taarifa za taasisi mbalimbali Wilaya ya Kongwa ikiwemo taarifa ya utekelezaji RUWASA, taarifa ya utekelezaji TFS, taarifa ya utekelezaji TARURA, taarifa ya utekelezaji TANESCO, Pamoja na taarifa ya utekelezaji DUWASA pia ziliwasilishwa.

Baadhi ya hoja ambazo zilitolewa ufafanuzi ni Pamoja na mnada mpya wa Visumi ambapo Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa na Diwani wa Kata ya Kongwa Mhe White Zuberi amefafanua kuwa mnada mpya wa Visumi utaendelea kusimamiwa vizuri na pia utawekwa pakilio la ng'ombe ili wafanyabishara waweze kununua na kusafirisha ng'ombe zao siku hiyo hiyo na kuwataka wafanyabishara wahamasishwe kujitokeza kwa wingi kufanya biashara katika mnada huo.



Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe Mayeka Simon Mayeka akijibu swali lililoulizwa na Mtendaji wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Kongwa kuhusu fidia ya maeneo ya Wananchi yaliyochukuliwa na Jeshi la Wananchi, amesema kuwa suala la fidia ya maeneo ya wananchi yaliyochukuliwa na Jeshi la wananchi wa Watanzania (JWTZ) yaliyopo katika Kitongoji cha Chimlata Kata ya Kongwa tayari linafanyiwa kazi na siku si nyingi Wananchi hao watalipwa fedha zao. Mh Mayeka pia amesisistiza kuwa maeneo hayo yaliyochukuliwa na Jeshi yapo katika mpango wa ulinzi wa Jeshi la wananchi wa Tanzania hivyo wananchi hawatakiwi kuendeleza shughuli zozote katika maeneo hayo.

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka S. Mayeka akizungumza katika Baraza la Madiwani.

Aidha baada ya kumpongeza mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa na timu ya afya kwa kufanya jitihada za ziada kupambana na mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu, Mh Mayeka amesisitiza kuwa suala la kipindupindu bado linasumbua katika baadhi ya maeneo hivyo amewataka Madiwani kusaidiana na idara ya afya kutoa elimu ya kipindupindu na utupaji taka ngumu ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa huo.

Kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mh Mayeka amewataka Viongozi hususani madiwani kuzuia mihemuko na viashiria vinavyoweza kupelekea uvunjifu wa amani katika jamii na ndani ya Nchi ili tuweze kudumisha Demokrasia tuliyonayo.

Kwa upande wake Mwenyekiti Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa dkt. Omary Nkullo Pamoja na Menejimenti kupitia Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi na walimu wote kwa ujumla wa Wilaya ya Kongwa wamepokea pongezi nyingi kwa matokeo ya Mtihani wa Taifa wa darasa la saba kwani kwa jitihada zao zimepelekea Wilaya ya Kongwa kuwa moja ya Wilaya vinara kwa ufaulu mzuri.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.