• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Baraza la Madiwani laweka Mikakati Kuongeza Mapato ya Ndani ya Halmashauri

Imewekwa: May 24th, 2018

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa laweka mikakati ya kuifanya Halamshauri yake kuwa Manispaa. Mikakati hiyo imewekwa kupitia Mkutano wa Baraza uliofanyika tarehe 23 Mei, 2018 ambapo wajumbe, watendaji na waalikwa walijadil changamoto za ukusanyaji mapato ya ndani na  njia za kuongeza mapato ya ndani ya Halmashauri.

Mweka Hazina wa Wilaya Ndugu Rumadha Mhando akiwasilisha taarifa ya Mapato na Matumizi kuishia mwezi Machi 31, 2018 kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji ameeleza kwamba, kwa kipindi cha Mwezi Julai 2017 hadi kufikia Mwezi Mei 20, 2018 Halamshauri ya Wilaya imefanikiwa kukusanya mapato ya jumla ya shs. 1,482,771,007.25 kutokana na vyanzo mbalimbali ambavyo ni sawa na 66.39% ya makisio ya mwaka yenye jumla ya shs. 2,233,593,000. Hadi sasa Halmashauri imetegemea makusanyo zaidi ya asilimia 75 lakini kutokana na changamoto za utoroshwaji mapato na upungufu wa vitendea kazi kumepelekea kutofikia lengo.

Aidha, ameeleza changamoto zingine ni upungufu wa watumishi katika zoezi la ukusanyaji wa mapato ambapo serikali iliagiza watumishi wa Halamshauri katika zoezi la ukusanyaji wa mapato ya ndani; baadhi ya vyanzo kuondolewa - kuchukuliwa na serikali kuu; elimu ndogo kwa wafanyabiashara na mgawanyo wa mapato katika Soko la Mazao la Kibaigwa.

Kwa upande wa utoroshwaji, ameeleza kwamba kumekuwa na utoroshwaji wa mapato katika eneo la Wilaya ya Kongwa kutokana na geografia ya wilaya kuwa na njia nyingi za kutokea,hivyo kufanya usimamizi kuwa mgumu. Katika changamoto hii, anasema utatuzi wake ni kufanya patrol ya mara kwa mara kwenye maeneo yote ya wilaya masaa 24. Hivyo, anaomba ushirikiano wa watendaji na wananchi kwa ujumla kufichua njia na watoroshaji ili mapato yasipotee.

Kuhusu upungufu wa vitendea kazi, mpaka sasa Halmashauri ina mashine za kielektroni za kukusanyia mapato (POS) 62 kati ya hizo POS 12 ni mbovu, 50 tu ndizo zinazofanya kazi. Hivyo, Halamshauri inahitaji POS 97 ili vijiji vyote pamoja na Mamlaka za Miji midogo za Kongwa na Kibaigwa ziwe na uwezo wa kukusanya mapato kwa kutumia mashine( Vijiji 87, Mamlaka Kongwa POS 5 na Kibaigwa POS 5).

Baada ya taarifa kuwasilishwa, Baraza lilisisitiza kwamba; Halamshauri kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya na wananchi washiriki kikamilifu katika kudhibiti mianya ya utoroshwaji mapato ya ndani - watendaji wa vijiji watimize majukumu yao na madiwani wawe sehemeu ya usimamizi; Halamshauri iongeze haraka POS zinazohitajika; elimu kwa wafanyabiashara na wananchi kuhusu sheria ndogo itolewe; 

Watendaji watoe umuhimu katika suala la ukusanyaji wa mapato ya ndani; Serikali iangalie namna ya kupata watendaji ili kuongeza nguvu kazi katika masuala ya ulinzi na usalama pamoja na ukusanyaji wa mapato katika ngazi za kata na vijiji; Halamshauri iongeze gari moja kwa Kitengo cha Ukusanyaji Mapato ili kurahisha shughuli za ufuatiliaji katika mageti na sehemu mbalimbali za ukusanyaji kama vile minadani, magulioni, n.k.

Aidha, Mwenyekiti wa Baraza, Mhe. White Z. Mwanzalilia amuomba Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Deogratius  Ndejembi  kuingilia kati pindi itakapobainika kwamba kuna hujuma zinafanyika kuhusu ukusanyaji wa mapato ya ndani na kuchukua hatua stahiki bila kusubiri taraibu za Baraza.

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa akihitimisha mjadala, ameeleza kwamaba atashirikiana na Halmashauri na atatumia mbinu zake anazozijua yeye katika kuwabaini watoroshaji wa mapato na atawachukulia hatua stahiki kwa mujibu wa sheria na hatamhurumia mtu yeyote atakayebainika kuwa na makosa.



Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.