Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Baraza la Wafanyakazi lajadili mafanikio na changamoto za kiutumishi

Imewekwa: December 22nd, 2023

Na Stephen Jackson, Kongwa DC

Baraza la Wafanyakazi la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa limejadili mafanikio na changamoto za Kiutumishi na kuishauri serikali kuzishughulikia kwa. Wakati.

Ushauri huo umetolewa na wajumbe mbalimbali wa Baraza, wakati wa majadiliano ndani ya kikao cha Baraza kilichofanyika  Desemba 22, 2023 katika ukumbi wa Elimu, chini ya Mwenyekiti wa baraza Bi. Paskalina Duwe Kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji (W) Dkt. Omary Nkullo. 

Awali, Baraza hilo  lilifanya uchaguzi wa Katibu baada ya Bwana Erasto Unambwe kumaliza muda wake, zoezi lililosimamiwa na Bi. Eunice Tesha, Afisa kazi Mfawidhi mkoa wa Dodoma. 

Katika uchaguzi huo Mwalimu Salome Nguvila wa Shule ya Sekondari White Zuberi, aliiibuka mshindi kwa nafasi ya katibu  kwa kura 25 kati ya 49 dhidi ya mshindani wake Bwana Erasto Unambwe aliyepata kura 24 ambaye kwa mujibu wa miongozo ameshika nafasi ya katibu msaidizi. 

Kufuatia matokeo hayo ya uchaguzi, Mwalimu Nguvila aliwashukuru wajumbe wote kwa  kumwamini na kuwaahidi kufanya kazi kwa ushirikiano na kwa kuzingatia Misingi ya utendaji kazi.

Naye Afisa kazi Mfawidhi, Mkoa Dodoma Bi. Eunice Tesha, licha ya kuwapongeza viongozi waliochaguliwa, pia alitumia fursa hiyo kufafanua dhana, umuhimu, muundo na wajibu wa kisheria wa Baraza la wafanyakazi. 

Akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Masuala ya kiutumishi,  kaimu Afisa Utumishi (W) Bwana Douglas B. John alisema Jumla ya Shilingi 147,000,000 zimepangwa kugharimia likizo za walimu 620 wa divisheni ya Elimu ya awali na msingi, huku shilingi 61,600,000 zikipangwa kugharamia likizo za walimu 218 wa divisheni ya Elimu Sekondari yenye jumla ya watumishi 537, na tayari 30,800,000.00 zimelipa watumishi 116, kwa likizo ya mwezi Juni, 2023 na shilingi 30,800,000.00 zitatumika kulipa watumishi 102, likizo ya mwezi Desemba. Kwa upande wa uhamisho wa walimu, hadi sasa shilingi 17,700,000.00 zimetumika kulipa walimu 27 waliohamishwa ili kukidhi mahitaji ya ikama. 

Kuhusu suala la Motisha kwa watumishi, taarifa hiyo inaonesha kuwa divisheni ya Elimu msingi na Sekondari imetenga Jumla ya Shilingi 4,000,000 kwa ajili ya watumishi watakaoingia kwenye orodha ya watumishi hodari kwa mwaka wa fedha 2023/2024 sawa na shilingi milioni mbili 2,000,000.00 kwa kila divisheni huku divisheni ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu yenye jumla ya watumishi 152 ikitenga shilingi 9,500,000.00

Aidha taarifa hiyo inseleza kuwa Katika kipindi cha Julai - Desemba, 2023, Jumla ya walimu 52 wameajiriwa na kupangiwa vituo vya kazi ambapo shilingi 130,290,000.00 zilitumika kulipa posho za kujikimu, na mwaka huu wa fedha jumla ya shilingi 35,000,000.00 zimetengwa kwa ajili ya uhamisho wa walimu. 

Akihitimisha taarifa hiyo, alisema jumla ya walimu 11 wanakabiliwa na mashauri ya kinidhamu 7 kati yao wakiwa ni walimu wa shule za Sekondari huku tuhuma zinazowakabili zikiwa ni utoro kazini pamoja na  mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi.

Akihoji hatua zilizochukuliwa kwa watumishi wenye tuhuma za mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi, Bi Zainabu Kudomu (Muuguzi) Kituo cha Afya Mlali alisema ni lazima hatua zichukuliwe ipasavyo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanafunzi husika wanafikishwa kwenye vituo vya Kutolea huduma za Afya ili wapimwe na ushahidi kuwasilishwa sehemu husika.

Kwa upande wake Mwalimu Samwel Malecela Mwenyekiti wa Chama Cha Walimu (CWT) Mkoa wa Dodoma, aliwataka viongozi wa Halmashauri kudhibiti urasimu kwa kuboresha utaratibu wa  kujibu hoja au barua za watumishi kwa wakati ili kuwaondolea usumbufu, huku akiomba utaratibu wa mazishi kwa watumishi ufanyiwe maboresho ambapo kiasi cha fedha kilichotengwa kwa ajili ya vifaa kama jeneza kitolewe kwa wafiwa ili wao waamue aina ya jeneza wanalohitaji. 

Katika Baraza hilo, Masuala ya kiutumishi ikiwemo huduma kwa wastaafu, na Uhamisho kwa watumishi yalijadiliwa msisitizo mkubwa ukiwekwa kwenye kuzingatiwa kwa maslahi ya kiutumishi. 

Akifunga kikao hicho, Mwentekiti wa Baraza Bi. Paskalina Duwe, amewashukuru wajumbe wote wa kikao na kuwahakikishia kuwa kutokana na usikivu na busara za Mkurugenzi wa Halmadhauri Dkt. Omary A. Nkullo, maazimio yote ya Baraza yatafanyiwa kazi. 

Baraza hilo lilihudhuriwa na wajumbe mbalimbali wakiwemo wawakilishi wa vyama vya wafanyakazi, wakuu wa divisheni na vitengo na uwakilishi wa watumishi ngazi mbalimbali. 


Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.