• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Baraza Maalumu Kongwa, lapitisha sheria Ndogo kudhibiti Sumu kuvu.

Imewekwa: June 2nd, 2022

Na Stephen Jackson

Baraza Maalumu la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa limepitisha sheria ndogo zitakazo tumika kudhibiti Sumu kuvu katika mazao ya Kilimo Wilayani hapa.

Mkutano huo wa baraza ulifanyika siku ya Alhamisi, tarehe 02 Juni, 2022 katika ukumbi wa Halmashauri ukihusisha Kamati kuu ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Madiwani, wakuu wa Idara na Vitengo, uwakilishi wa Mahakama, vyama vya siasa na wadau mbalimbali.

Sumu kuvu ni aina ya sumu inayopatikana kwenye Mazao kama vile mahindi, karanga, pamba na kadhalika, ambayo athari zake kwa binadamu ni kusababisha saratani ya ini.

Kwa mujibu wa shirika la Afya Duniani (WHO), sumu kuvu huharibu karibu au zaidi ya asilimia 25 ya chakula kinachozalishwa duniani kila mwaka.

Kwa kuzingatia Maelezo ya Viongozi wa baraza hilo, sheria hizo zimetungwa kutokana na Wilaya ya Kongwa kupatiwa mradi mkubwa wa Kilimo wenye thamani ya TZS.  Bilioni kumi na tisa unatekelezwa katika Kijiji cha Mtanana.

Sheria hizo zilizotungwa chini ya kifungu cha 153(1)(b) Cha Sheria ya serikali za Mitaa (Mamlaka ya Wilaya) Sura ya 287, zimepitishwa na baraza hilo chini ya Mwenyekiti wake Mhe. White Zuberi Mwanzalila na Katibu  wake Dkt. Omary Nkullo.

kupitishwa kwa sheria hizo ni hatua muhimu inayoruhusu mchakato huo kuendelea katika hatua na Mamlaka nyingine hadi hapo zitakapotangazwa katika gazeti la Serikali ili zianze kutumika.

Kufuatia Hatua hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius Mwema Emmanuel, amepongeza mchakato huo kwa kuwa utasaidia kuleta tija katika sekta ya kilimo wilayani Kongwa. 

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. White Zuberi Mwanzalila, ametoa wito kwa wadau kuchangamkia fursa za uwekezaji kwenye eneo linalozunguka mradi huo.

Miongoni mwa Mambo yatakayo simamiwa na Sheria hizo ni pamoja na Uaandaji, Uvunaji, Usindikaji, Usafirishaji na uhifadhi wa Mazao ya kilimo.

Aidha, sheria hizo ndogo, zinampa Mamlaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kufifilisha makosa kwa kumtoza faini isiyozidi laki tatu na isiyopungua laki moja, mkulima atakaye kwenda kinyume.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.