• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Benki Kuu ya Tanzania (BoT) yatoa Mafunzo ya Utambuzi wa Noti Bandia Wilayani Kongwa

Imewekwa: May 26th, 2017

Benki Kuu ya Tanzania imeanza kutoa mafunzo ya utambuzi wa noti bandia kwa watu wote Wilayani Kongwa ili kuepuka kupokea au kufanya matumizi kwa kutumia noti Bandia. Mafunzo haya yametolewa na maafisa toka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ambapo wajumbe waliohudhuria kikao cha maandalizi ya “Mbio za Mwenge wa Uhuru 2017” Wilayani Kongwa. Katika Semina hii fupi, mada hizi zimewasilishwa; Huduma za Kibenki (kuagiza, kutoza na kutunza sarafu na noti); Kutambua Alama za Noti - ili kuzuia kusambaa kwa noti bandia; na Elimu Kuhusu Hundi.

KUHUSU UTAMBUZI WA NOTI BANDIA:

Wataalam wametoa ufafanuzi kuhusu alama mbalimbali ambazo mtu anaweza kutumia katika kutambua fedha halali kwa matumizi na fedha bandia katika noti za shilingi; 500; 1,000; 2,000; 5,000 na 10,000. Zipo njia tatu za kuweza kutambua noti kuwa ni halali au bandia, ambazo ni;

Njia ya Kwanza: Kuona kwa Macho:-

  • Angalia kivuli (water mark) yenye picha ya Baba wa Taifa
  • Angalia alama ya mistari – kwa noti halali inaakisi (reflects)
  • Angalia picha ya twiga nyuma ya noti – iwe na rangi ya dhahabu inayoakisi – reflects

Njia ya Pili: Kupapasa:-

  • Papasa alama ya maua pembeni mwa noti – isipokwaruza siyo fedha halali.
  • Papasa maneno yaliyopo chini ya maneno ya “BENKI KUU YA TANZANIA” – yawe yanakwaruza.
  • Papasa alama ya “V” kwa noti za 1000, 2000, 5000 na 10,000; na “mistari (=)” kwa noti ya shilingi 500 – alama hizi zinakwaruza kwa noti halali.

Njia ya Tatu: kutumia Kifaa Maalum:-

Tumia taa yenye mwanga maalum kuweza kutambua alama ambazo zinaakisi ukizimulika, Kama ifuatavyo;

  • Mulika kwenye kivuli (water mark) cha Baba wa Taifa utaona kisanduku na thamani ya fedha husika – kama huoni hivyo si fedha halali.
  • Mulika chini ya picha ya twiga, utaona maua – kama hayaonekani si fedha halali.
  • Mulika namba za fedha zitaakisi – Kama haziakisi si fedha halali.
  • Aidha, waweza kutumia kioo cha lenzi yenye nguvu kusoma maneno yote yaliyoandikwa, lakini kwa fedha bandia hayawezi kuonekana.\

KUHUSU FEDHA ZILIZOCHAKAA:

  • Katika mada hii, Afisa wa Benki Kuu ya Tanzania anaeleza kuhusu sifa za kuweza kubadilisha fedha iliyochakaa, ambazo ni;
  • Fedha isiwe bandia;
  • Fedha iwe na asilimia sabini na tano (75%) ya ukubwa wake;
  • Maneno yaliyoandikwa “Fedha halali ya Malipo ya shilingi …” yawe zaidi ya nusu ya maneno yanatakiwa kuwepo; na
  • Fedha lazima iwe na sahihi mbili zilizokamilika.

KUHUSU UTUNZAJI WA NOTI:

Maafisa wa BoT wasema kwamba fedha zote ni muhimu kutunzwa kwani zinatengenezwa kwa gharama kubwa, hivyo kuharibu ni kulitia hasara taifa. Hivyo, BoT inawataka wananchi wote kutunza fedha za noti kwenye “wallets” au “pochi” kwa akina mama. Aidha, Afisa wa BoT anasema kuwa kuchakaza fedha (note au sarafu) ni kosa kisheria.

Waliopata mafunza haya watakiwa kutoa mafunzo kwa wengine, aidha maafisa hao watakuwa wkitembea maeneo mbalimbali kutoa mafunzo kuhusu utambuzi wa noti kwa wananchi wote, na kuwataka wafanyabishara wakubwa na taasisi zinazopokea fedha nyingi kuwa makini na kuzingatia alama za utambuzi.

Taarifa na Nkinde Moses (Afisa TEHAMA Wilaya ya Kongwa)

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.