• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

DC KONGWA AGAWA VYETI KWA WAHITIMU VETA WANAWAKE NA SAMIA

Imewekwa: August 31st, 2025

DC KONGWA AGAWA VYETI KWA WAHITIMU VETA WANAWAKE NA SAMIA

Na Bernadetha Mwakilabi

Habari – Kongwa DC

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka Simon Mayeka amegawa vyeti kwa wahitimu 227 wa Chuo cha Veta Kongwa waliopatiwa mafunzo ya fani mbalimbali chini ya mpango wa mafunzo kwa ushirikiano kati ya Veta na “Wanawake na Samia.“

Akiongea katika mahafali hayo, Mhe Mayeka amesema kuwa kuwepo kwa mafunzo hayo ni ushahidi wa utekelezaji wa sera za awamu ya sita chini ya Rais Samia na ni matokeo ya dira ya Serikali kujenga uchumi wa ushindani kupitia Veta.

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka akiongea na wahitimu wakati wa kufunga mahafali hayo.

Licha ya kuwataka wahitimu kutumia vizuri fursa ya ujuzi walioupata lakini pia Mhe Mayeka amesema wanawake wakiwezeshwa jamii inaimarika hivyo wawezeshwe kwa kupata zabuni na mikopo ya Serikali ili waweze kuwa mabalozi wazuri wa ufundi stadi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Veta Kanda ya Kati Bw. Ramadhani Mataka ameeleza kuwa Veta ina jukumu la kutoa mafunzo ya ufundi stadi na ujuzi mbalimbali hivyo ni vyema wahitimu kutumia ujuzi wao vizuri ili kuleta mabadiliko katika jamii.

Mkurugenzi wa Veta Kanda ya kati bw. Ramadhani Mataka akiongea wakati wa mahafali hayo.

Akimuwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa, Bi. Faraja Kasuwi amewatoa hofu wahitimu kuwa uwepo wa mikopo ya asilimia kumi ya mapato ya Halmashauri ambapo asilimia nne kati ya fedha hizo ni kwa ajili ya kuwawezesha wanawake hivyo changamoto ya kupata mitaji haitakuwepo tena.

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa bi Faraja Kasuwi akizungumza katika mahafali hayo.

Nae Mkuu wa Chuo cha Veta Kongwa Bw. Abdulkadir Yusuf amefafanua kuwa mafunzo hayo kwa wanawake na Samia yamegharamiwa na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi kwa asilimia mia moja na baada ya awamu hii kuhitimika awamu ya pili itafuata ili kusaidia wanawake kujiajiri.

Mkuu wa chuo cha Veta Kongwa Bw. Abdukadir Yusuf.

Aidha Bi. Fatma Madihi Mwenyekiti wa Wanawake na Samia Taifa ameomba Serikali kuwapatia vitendea kazi kama Vyerehani ili kuendeleza walichojifunza, kuwawezesha kupata tenda mbalimbali za Serikali na kupatiwa mikopo.

Mwenyekiti wa wanawake na samia Taifa Bi. Fatma Madihi akizungumza na wahitimu.

Kwa upande wao wahitimu wametumia nafasi hiyo kumshukuru Mhe. Rais Samia, Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Viongozi wa Wilaya ya Kongwa na viongozi wote wa Wanawake na Samia kwa kuwezesha mafunzo hayo yakiwemo ya udereva, ususi, upambaji, ujenzi, ushonaji, upishi na kompyuta.

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili September 02, 2025
  • Tangazo la nafasi ya kazi June 13, 2025
  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • DC KONGWA AGAWA VYETI KWA WAHITIMU VETA WANAWAKE NA SAMIA

    August 31, 2025
  • MAGEREZA KONGWA YAJIVUNIA MIAKA 64 YA UREKEBU KWA WAFUNGWA

    August 30, 2025
  • JUKWAA LA KUTETEA USTAWI WA MNYAMAKAZI PUNDA KUANZISHWA KONGWA

    August 29, 2025
  • KOFIH YAKABIDHI VIFAA NA MIUNDOMBINU YA AFYA KONGWA

    August 24, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.