• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

DC Kongwa aonya wafanyabiashara wanaoficha au kukiuka bei elekezi ya sukari

Imewekwa: January 31st, 2024

Na Stephen Jackson, Kongwa DCM

kuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka Simon Mayeka, amewataka wafanya biashara wa Sukari kuuza bidhaa hiyo kwa kuzingatia bei elekezi ya serikali  ili kuwawezesha wananchi kumudu gharama za bidhaa hiyo inayodaiwa kuadimika. "Toeni sukari kama ipo uzeni hata kama ni kwa faida ndogo, wapeni wananchi wanywe chai"

 Mhe. Mayeja alitoa agizo hilo Januari 31, 2024, kwa wafanyabiashara wenye maduka yanayouza sukari jumla na rejareja Wilayani Kongwa, alipoitisha kikao maalumu kufuatia dalili za kuadimika kwa sukari kulikopelekea baadhi ya wafanya biashara kutozingatia bei elekezi ya serikali huku wengine wakificha bidhaa hiyo na kupelekea usumbufu kwa wananchi. "Juzi nilimtuma dereva wangu dukani akaninunulie sukari. Hadi mimi mwenyewe nimekosa sukari"  alinukuliwa Mayeka.

Yote hayo yamejiri kufuatia mazungumzo baina yao na Kamati ya usalama ya Wilaya na Maafisa biashara wa Halmashauri kupitia kikao maalumu kilichoitishwa na mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka Simon Mayeka Januari 31, 2024 ofisini kwake.

Wakitoa michango yao baadhi ya Wafanya biashara walisema, bei elekezi iliyotolewa na Serikali hivi karibuni imewaathri baadhi ya wafanya biashara wa Jumla na rejareja kwani tayari walikuwa wameshanunua sukari hiyo kwa bei ya juu hivyo kuna uwezekano wa kuficha sukari kutokana na  kushindwa kuuza kwa bei elekezi agizo, linalodaiwa kuwapa hasara.

Priscus Shirima mfanyabiashara mashughuli Mjini Kongwa, alisema upo uhaba wa sukari nchini kutokana na viwanda vya ndani kupunguza uzalishaji kipindi cha masika hivyo ameiomba serikali kuimarisha upatikanaji wa sukari nchini hasa kwa kipindi cha masika ili kukabiliana na changamoto hiyo.

 Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Afisa biashara Wilaya ya Kongwa Bwana Yonaza Mchome alisema, ni wajibu wa wafanyaniashara kuzingatia bei elekezi na si vinginevyo kwani ofisi ya biashara itafanya msako mkali katika maduka na kuwachukulia hatua wote watakaobainika kuuza sukari nje ya bei elekezi.

Hata hivyo kupitia kikao hicho, Jeshi la Polisi Kongwa limeahidi kushirikiana na wataalamu wa biashara na wadau wengine kufanya msako mkali katika maduka  ili kuwabaini wafanya biashara wanaoficha sukari kwa lengo la kuuza  kinyemela na kuwachukulia hatua za kisheria.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.