• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

DC Kongwa ahimiza wafanya biashara kulipa Kodi.

Imewekwa: August 12th, 2022

Na Stephen Jackson, Kongwa.

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius Mwema Emmanuel, amewataka wafanya biashara kutoa ushirikiano kwa kufuata sheria ya ulipaji kodi ili waweze kufanya biashara katika mazingira rafiki.

"Sijaja hapa kusema wafanya biashara msilipe Kodi. Nataka mlipe kodi, lakini mfuate taratibu pia Kwa sababu suala la Kodi, lipo Kisheria pia". Alisisitiza Mhe. Emmanuel.

Wito huo ulitolewa tarehe 12 Agosti, 2022 wakati wa kikao Maalum baina ya  wafanya biashara wa Mamlaka ya mji mdogo wa Kibaigwa na viongozi wa Serikali ngazi ya wilaya kilichoitishwa  Kwa lengo la kusikiliza kero.

Katika kikao hicho, Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Wilaya ya Kongwa Bi. Sophia Boma,  amewahimiza wafanya biashara kutambua umuhimu wa kutumia mashine za kielektroniki "EFD" katika utoaji wa risiti.

Bi. Sophia Boma,  alieleza kuwa utoaji risiti kwa njia ya EFD unamsaidia mfanya biashara kutunza kumbukumbu sahihi za mauzo, na hivyo kurahisisha ukusanyaji wa Mapato ya Serikali.

"Ni kitu ambacho kipo Kisheria, Sasa hivi mnatakiwa mtumie mashine kutolea risiti ili kusiwe na haja ya ofisa kuja huko. Mimi nikiwa ofisini nikaingia kwenye akaunti yako ya EFD niweze kuona mauzo unayoyafanya". Alisema Bi. Sophia.

Katika kikao hicho, wamiliki wa biashara waliainisha kero kadha wa kadha zinazowakabili na kuiomba Serikali kuzitafutia ufumbuzi kupitia Mamlaka zenye dhamana.

Miongoni mwa kero zilizowasilishwa ni pamoja na zuio la kufungua biashara siku za Jumamosi asubuhi lililotafsiriwa kama shinikizo kwa wafanya biashara kushiriki zoezi la usafi wa Mazingira, hoja iliyoibuliwa na mfanya biashara Irene Kimenye.

Akijibu kero hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Dkt. Omary Nkullo, alibainisha kuwa uamuzi  huo tayari ulikwisha tenguliwa kwenye kikao Maalum, na kwamba si kosa kwa mjasiriamali kufungua biashara yake huku akiendelea na zoezi la usafi.

"Hivi Kuna ubaya gani Mimi nifanye usafi halafu biashara yangu ikiwa wazi. Kwa sababu Kuna "nature" ya biashara zingine ukifunga mpaka saa nne, umeshakosa wateja". Alisema Dkt. Nkullo.

Kwa upande mwingine, wafanya biashara wameiomba "TRA" kuboresha mifumo yake ili kuwaondolea usumbufu sambamba na kutoa elimu kwa mlipa kodi, kufanya kazi kwa kuzingatia utu na kuboresha huduma kwa mteja.

Naye Meneja wa shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Wilaya ya Kongwa Mhandisi Evodius Kagaruki Mkiza, alijibu hoja ya kukatika Kwa umeme mara Kwa mara kuwa zipo sababu mbalimbali za kukatika Kwa umeme hivyo ni vema wananchi kujenga utamaduni wa kutoa taarifa huku akiwahakikishia kuwa shirika linaendelea na jitihada za kuboresha miundombinu ili kuondokana na tatizo hilo.

Kikao hicho Maalum, kilifanyika katika ukumbi wa St. Pio Kibaigwa baada ya Mkuu wa Wilaya Kupokea ombi la Mhe. Diwani wa Kata hiyo Mhe. Chande H. Mrisho  la kuitisha kikao Cha kusikiliza kero za Wajasiriamali.


Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.