• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

DC KONGWA KUNUSURU ZAIDI YA HEKARI 600 ZA MISITU.

Imewekwa: January 14th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mheshimiwa Mayeka Simon Mayeka amezuia shughuli zote za kibinadamu zilizokuwa zikifanyika katika maeneo ya hifadhi ya mazingira katika misitu iliyopo katika safu za milima ya Tangalata mpakani mwa Kijiji cha Mbagilwa Kata ya Ng'humbi kutokana na uharibifu mkubwa wa Mazingira unaoendelea katika milima hiyo.

Akifanya ukaguzi katika milima hiyo Mhe. Mayeka akiwa ameambatana na wataalamu mbalimbali wa Mazingira amewaagiza viongozi wa Kata ya Ng'humbi kuhakikisha wavamizi hao wanarudisha maeneo yote ya hifadhi ya mazingira ili kuyalinda ipasavyo maeneo yenye vyanzo vya maji Kwa faida ya wananchi kwani maji ni maisha na ni uhai.

Aidha Mhe. Mayeka ameeleza kuwa pamoja na kuzuia shughuli hizo zikiwemo za kilimo, kulisha mifugo na ukataji miti kiholela lakini pia anahitaji uongozi wa vijiji vya Ng'humbi na Mbagilwa kuwasilisha majina yote ya watu waliofanya uharibifu katika maeneo hayo ili wachukuliwe hatua za kisheria za uharibu wa mazingira.

Vilevile Mhe. Mayeka ameagiza wakala wa misitu Tanzania (TFS) wilaya ya Kongwa kuweka doria kuhakikisha hakuna mtu anaengia kufanya shughuli yoyote katika misitu na kuhakikisha kuwa mazao yote yaliyopandwa katika milima hiyo yasiguswe wala kuendelezwa bila kibali maalum kutoka kwake.

Bwana Farouk Isa ambaye ni Mtendaji wa Kata ya Ng'humbi ameweka wazi kuwa waharibifu wengi wa Mazingira katika msitu huo wanatoka katika Kijiji Cha Mbagilwa, jambo lililompelekea kuomba usaidizi wa vyombo vya ulinzi na usalama ili kudhibiti uharibifu huo kutokana na mazingira magumu ya eneo hilo kwani wahusika wanajulikana na wamekuwa wakaidi.

Kwa upande wake Afisa Uhifadhi wa misitu (TFS) Bwana Patrick Mbughi amesema kuwa milima hiyo ina vyanzo vya maji vitatu lakini athari zilizofanywa na uharibifu huo zimepelekea kukauka kwa baadhi ya vyanzo vya maji na kusombwa kwa madaraja katika Kijiji cha Ng'humbi jambo linalosababishwa na maji mengi ambayo yamekuwa yakishuka kwa kasi kutoka milimani.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.