Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

DC Mayeka ahimiza usafi na uhifadhi wa Mazingira

Imewekwa: January 16th, 2024

Na Stephen Jackson, Kongwa DC

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka Simon Mayeka amewataka wananchi kushiriki kwenye shughuli za utunzaji wa mazingira ikiwa ni pamoja na usafi wa kila jumamosi na upandaji miti katika maeneo yao.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa zoezi la upandaji miti lililofanyika Januari 16, 2024 Mhe. Mayeka amezielekeza taasisi mbalimbali Wilayani Kongwa kuwa na mipango ya muda mrefu ya matumizi ya ardhi, itakayowezesha taasisi  hizo kutunza miti inayopandwa katika maeneo hayo.

Akizungumzia kampeni ya usafi kwa siku za Jumamosi, amesema Wilayani kongwa kwa sasa usafi unafanyika Kila Jumamosi badala ya Jumamosi ya mwisho wa mwezi kama ilivyopangwa  kitaifa.

Aliongeza kuwa, kwa mujibu wa taratibu, Wananchi waliopakana na barabara wanawajibika kusafisha hadi barabarani na pia katika siku za usafi wa Mazingira wafanya biashara hawana sababu ya kufunga maeneo yao ya biashara kwani kinachotakiwa ni kuhakikisha mazingira yanayowazunguka yanakuwa katika hali ya usafi. "Kwa kuona umuhimu, kuna siku atafunga duka yeye mwenyewe ili akafanye usafi" Mhe. Mayeka.

Kupitia hafla hiyo Mayeka ametoa wito kwa jamii na taasisi za umma kuachana na mazoea ya kupanda miti mingi kwa pamoja pasi na mikakati thabiti ya kuitunza., hukuakipiga marufuku ukataji holela wa miti pasipokuwa na vibali. " Vibali vya kukata miti vinatolewa na Ofisi ya mkuu wa Wilaya au kwa Watendaji wa kata kwa niaba." Alisema Mayeka.

Katika Mazungumzo yake Mhe. Mayeka alizitaka  taasisi zote za umma kutekeleza agizo la upandaji miti kama ilivyoazimiwa ili wananchi waweze kuhamasika na kuunga mkono jitihada za serikali katika uhifadhi wa mazingira.

Naye  Dkt. Omary A. Nkullo Mkurugenzi Mtendaji (W) alisema Halmashauri imekusudia kupanda miti kwenye eneo lote la Hospitali ya Wilaya lenye ukubwa wa ekari 21, kwa kuwa ipo miche ya kutosha ambapo zaidi ya miti 200 imepandwa katika hafla hiyo.

Akizungumza kikao hicho, afisa Maliasili na mazingira bwana Godfrey Mujairi alitaja shughuli za kibinadamu kama changamoto kubwa inayopelekea uharibifu wa Mazingira ikiwemo uvamizi wa misitu na maeneo ya uchimbaji madini, ukataji miti ovyo, kilimo na ufugaji holela na utupaji hovyo  taka kando ya barabara.

Zoezi la upandaji miti limehusisha kamati ya usalama ya Wilaya, Wakuu wa Divisheni naVitengo, wananchi na watumishi ambapo Mhe. Mayeka alipanda mti kama ishara ya uzinduzi wa zoezi.


Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.