• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

DC Mayeka Aiasa Jamii kushiriki Malezi bora ya Watoto na Wazee

Imewekwa: June 14th, 2024

Na Stephen Jackson, Kongwa DC

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka Simon Mayeka ameitaka Jamii kuzingatia Suala la Malezi bora ya watoto katika familia ili kujenga Jamii yenye maadili mema.

Mayeka amesema hayo wakati akihutubia Kongamano maalumu la Maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika lililofanyika shule ya Sekondari Kibaigwa Juni 14, 2024.

Aidha amesema  wazazi wanao wajibu wa kuwalinda watoto wao dhidi ya athari za utandawazi kwa kudhibiti matumizi ya vifaa vya teknolojia zikiwemo luninga na simu za mikononi.

"Turudi tulikotoka, huu utandawazi si kila kitu ni sahihi"

Kuhusu Malezi ya Wazee, Mayeka amesema Wazee wamelitumikia taifa kwa uadilifu hivyo Jamii inalo jukumu la kuwatunza kwa upendo pasipo kinyongo huku wakiwalinda dhidi ya vitendo vya kikatili na kuvitolea taarifa pindi vinapobainika.

Ameongeza kuwa Jamii nzima inao wajibu wa kuwahudumia Wazee na kuwasaidia kupunguza changamoto mbalimbali za kimaisha ikiwemo kuwavusha barabara, kuwasikiliza, kuwapa huduma Bora za Afya, kuwapa kipaumbele katika mambo mbalimbali na kuwapa heshima wanayostahili.

"Madhara ya kutoheshimu Wazee ni kuongezeka kwa ukiukwaji wa Maadilili" Mhe. Mayeka.

Ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa wazazi kukuza ushirikiano na walimu kwa kushiriki vikao vinavyoitishwa ili waweze kujadiliana kuhusu maendeleo ya watoto.

Akizungumza kwa niaba ya Wazee, Mwenyekiti wa Wazee Wilaya ya Kongwa,  Mwalimu Eliney Mathayo Sogodi ameomba Serikali kuwezesha Wazee kupata huduma wanazostahili kama ilivyo kwenye miongozo ikiwemo kupewa matibabu bure na kuwa vipaumbele katika foleni za matibabu, sambamba na kutenga bajeti za kuwawezesha kufanya vikao na mabaraza ya Wazee kwa mujibu wa Sheria huku akisisitiza kutiliwa mkazo kwa Mabaraza ya shule na vipindi vya dini shuleni.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Kongwa Bi. Paskalina Duwe alisema miongoni mwa sababu za kuadhimisha  siku ya mtoto wa Afrika katika Mamlaka ya Mji Mdogo Kibaigwa ni pamoja na kuwepo kwa matukio mengi ya ukatili dhidi ya Watoto unaochangia kuwepo kwa watoto wasio na maadili wajulikanao kama Panya kalowa.

Akiwakilisha Dawati la Jinsia, Mwendesha Mashtaka wa Polisi D/CPL Adra Rwechungura kutoka Jeshi la Polisi Kongwa alitoa wito kwa Wananchi kushirikiana na Jeshi hilo kufichua uhalifu na kuwa tayari kutoa ushahidi ili watuhumiwa wa vitendo vya ukatili waweze kuchukuliwa hatua. " Vitendo vya ukatili vipo vingi sana Kibaigwa vipo juu sana kwa Wilaya ya Kongwa" Alisema Adra.

Katika Maadhimisho hayo, wanafunzi wa shule ya msingi Mkoka na Kibaigwa walipata fursa ya kufikisha jumbe mbalimbali zinazohamasisha upatikanaji wa haki za watoto kupitia nyimbo na mashairi na kuchangia hoja mbalimbali kwenye Kongamano kuhusu wajibu wa wazazi katika Malezi ya watoto.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.