• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

DC Mayeka arejesha ekari 1,705 kwa Wananchi Kata ya Mlali.

Imewekwa: May 31st, 2024

Na Stephen Jackson, Kongwa DC

Mamlaka ya Huduma za Misitu TFS imerejesha jumla ya Ekari 1705 kwa Serikali za  vijiji vya Mlali Bondeni na Mlali Yegu vilivyopo Kata ya Mlali Wilayani Kongwa.

Tamko la kurejeshwa kwa maeneo hayo limetolewa na Mhe. Mayeka Simon Mayeka, Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mei 31, 2024 wakati akihutubia mikutano ya hadhara katika vijiji hivyo.

Katika hotuba yake Mhe. Mayeka Alisema jumla ya ekari 608 zimerejeshwa kwa ajili ya Wananchi wa Kijiji cha Mlali Bondeni wakati ekari 1097 zikirejeshwa kwa wakazi wa Kijiji cha Mlali Yegu.

Akitoa masharti ya kurejeshwa kwa Ardhi hiyo Mhe. Mayeka alisema, jumla ya ekari 852.5 sawa na nusu ya eneo zima la ardhi iliyorejeshwa, zitapaswa kuhifadhiwa na vijiji hivyo kwa ajili ya matumizi ya umma, na amewataka Wananchi kuepuka uharibifu wa Mazingira unaosababishwa na shughuli za kibinadamu katika maeneo hayo.

Mhe. Mayeka kwa niaba ya Serikali amerejesha Ardhi hiyo kufuatia kilio cha muda mrefu cha Wananchi wa Kata hiyo kudai maeneo yao yaliyochukuliwa taasisi ya Hifadhi ya Misitu Dodoma (HADO) na baadayeTanzania Forest Service (TFS).

Aidha DC Mayeka amesikiliza kero za Wananchi wa vijiji hivyo ikiwemo migogoro ya Ardhi, mapato na matumizi, na changamoto binafsi.

Kufuatia kero hizo Mayeka amewataka Wananchi kushiriki mikutano halali ya vijiji kwa ajili ya kusomewa mapato na matumizi,  na kukemea ubadhirifu wa fedha za umma ikiwemo fedha za miradi ya maji.

Ili kudhibiti changamoto hizo Mayeka amewaasa Wananchi kutumia fursa ya uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za mitaa na Vijiji kuchagua viongozi bora watakaosimamia maslahi ya umma badala ya kujinufaisha wao.

Kuhusu kero ya miradi ya maji ameshauri kuundwa kwa vyombo vya watumia maji ili kudhibiti mianya ya upotevu wa fedha zitokanazo na miradi ya maji, ili kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji kwa Wananchi.

Wakitoa kero mbalimbali mbele ya Mkuu wa Wilaya Wananchi wa vijiji vya Mlali Bondeni na Mlali Yegu wameomba Mhe. Mayeka kushughulikia kero hizo, jambo ambalo Mayeka amelipokea na kuwaasa kuzingatia taratibu za uwasilishaji kero na malalamiko kuanzia ngazi ya chini badala ya kuruka ngazi mbalimbali za ushughulikiwaji wa kero zao.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.