• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

MAAFISA KILIMO WAMEAGIZWA KUWASAJILI WAKULIMA ILI WAWEZE KUPATA MBEGU ZA RUZUKU

Imewekwa: October 8th, 2025

MAAFISA KILIMO WAMEAGIZWA KUWASAJILI WAKULIMA ILI WAWEZE KUPATA MBEGU ZA RUZUKU

Na Bernadetha mwakilabi

Habari – kongwa DC

Maafisa Kilimo Wilayani Kongwa wameagizwa kuhakikisha wanawaandikisha na kuwasajili wakulima wote na kuwapatia namba zitakazo wawawezesha kununua mbegu za ruzuku.

Ndg. Dotto Massato Afisa Kilimo Kata ya Lenjulu akifafanua suala la upatikanaji wa mbegu za ruzuku

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka Simon Mayeka alipokuwa akiongea na wananchi wa Kijiji cha Lobilo kilichopo kata ya Lenjulu Tarafa ya Mlali katika mkutano wa hadhara wa kutambua na kuzitatua changamoto za wananchi wa Kijiji hicho.

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka akisikiliza changamoto za wananchi wa Lobilo.

Hata hivyo wananchi hao wameipongeza ofisi ya TANESCO wilaya ya Kongwa kwa kuwahakikishia umeme wa uhakika lakini pia wamebainisha changamoto kadhaa zinazowakabili.

Akijibu hoja ya changamoto ya miundombinu ya barabara Kaimu Meneja wa wakala wa barabara vijijini (TARURA) Wilaya ya Kongwa Mhandisi Mashaka Ngeleja amesema kuwa barabara ya kutoka Pandambili kwenda Lenjulu hadi Kiteto mkandarasi amepatikana anasubiri fedha ili kuanza kazi, na barabara ya kutoka Lobilo kwenda Laiseli itaingizwa katika bajeti ya mwezi Novemba mwaka huu.

Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini Mhandisi Mashaka Ngeleja akijibu hoja za miundombinu ya Barabara katika mkutano huo.

Aidha kwa upande wake kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Ndg. Hassan Hamis wakati akijibu hoja ya ukosefu wa Zahanati amesema kuwa kwa sasa wanatumia huduma ya Kliniki Mkoba ambapo mhudumu wa afya anatoka kituo cha afya kwenda kutoa huduma kwenye kijiji kisichokuwa na zahanati mara mbili kwa mwezi, lakini mpango wa Serikali kuwajengea zahanati upo hivyo Serikali ya Kijiji iandae eneo lisilopungua hekari 10 kwa ajili ya kuanza ujenzi.

Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Ndg. Hassan Hamis akijibu hoja za afya katika mkutano huo

Hata hivyo nae Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka ametolea ufafanuzi wa suala la changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama kuwa mpaka ifikapo mwishoni mwa mwezi Oktoba 2025 mkandarasi atakuwa amefika kijijini hapo kuchimba kisima ili waweze kupata huduma hiyo.

Licha ya kusisitiza suala la elimu kwa Watoto na kutunza na kulinda miundombinu ya Serikali kama vile umeme, maji na shule pia Mhe. Mayeka ameitaka Serikali ya Kijiji cha Lobilo kuweka vizuri mipaka ya Kijiji na matumizi ya ardhi ili kuepukana na migogoro.

Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Lobilo wakiwa katika mkutano.

Samabamba na hayo Mhe. Mayeka ametumia mkutano huo kuwakumbusha wananchi kulinda na kuitunza amani waliyonayo katika kipindi hiki cha kampeni na kuelekea uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani.

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kazini September 23, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili September 02, 2025
  • Tangazo la nafasi ya kazi June 13, 2025
  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • DED KONGWA AZINDUA DARASA JANJA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA KIBAIGWA

    October 09, 2025
  • TRA KONGWA WAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA

    October 09, 2025
  • DC KONGWA AKAGUA MIRADI YA ELIMU KATA YA LENJULU

    October 08, 2025
  • MAAFISA KILIMO WAMEAGIZWA KUWASAJILI WAKULIMA ILI WAWEZE KUPATA MBEGU ZA RUZUKU

    October 08, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.