• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

DUWASA NA VEI WAKABIDHI MAHITAJI YA SHULE KWA WATOTO 105.

Imewekwa: June 13th, 2025

Mamlaka ya Maji Safi na usafi wa mazingira (DUWASA) kwa kushirikiana na shirika la VEI (Dutch Water Operating) wametoa msaada wa sare za shule na vifaa vya kujifunzia kwa wanafunzi 105 wa shule za msingi saba za Kata ya Kibaigwa Wilayani Kongwa lengo ikiwa ni kutoa sehemu ya mapato yao kwa jamii inayowazunguka yenye uhitaji.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi vifaa hivyo Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mheshimiwa Mayeka Simon Mayeka amewataka wazazi na walezi kuacha tabia ya kuwaambia watoto wajifelishe kwenye mitihani yao ili kukatisha masomo yao kwa lengo la kukwepa majukumu kuwapatia mahitaji ya shule ikiwemo manunuzi ya sare za shule.

Mhe. Mayeka amesema kuwa ni jambo la kusikitisha kuona wazazi wanakata tamaa ya kupeleka watoto shule kwa ajili ya ukosefu wa mahitaji ya shule badala ya kutafuta njia ya kuwasaidia ili iwafikie malengo yao.

Aidha, Mhe. Mayeka ameeleza kuwa Wilaya ya Kongwa hutenga kiasi cha shilingi milioni 20 kila mwaka kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi wanaoishi katika mazingira magumu ili kuwasaidia wanafunzi kupata elimu bila vikwazo.

Nae Katibu Tawala Wilaya ya Kongwa Bi. Sozi Ngate ameeleza kuwa jukumu la wazazi ni kuhakikisha wanawafikisha watoto wao shuleni ili kupata elimu na amewakumbusha wazazi kuona umuhimu wa elimu kwa watoto, jamii na Taifa kwa jumla.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa DUWASA Mkoa wa Dodoma Bi. Rachel Muhando amesema kuwa taasisi yao inatambua wajibu wa kushirikiana na Serikali na jamii katika kuunga mkono jitihada za kielimu kwa watoto wa kitanzania ndiyo sababu ya kutoa mahitaji kwa watoto hao.

Akimuwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa, Mwalimu Masta Mwashala ameziomba taasisi nyingine ziige mfano uliofanywa na DUWASA pamoja na VEI kwa kusaidia makundi yenye uhitaji katika jamii hususani wanafunzi ili kufanikisha safari zao za kielimu.

Aidha mwl. Mwashala ameeleza kuwa zaidi ya watoto 450 Wilayani Kongwa wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa mahitaji ya shule hivyo kwa Msaada uliotolewa kwa watoto hao 105 ni hatua ya matumaini kwa kundi hilo lenye uhitaji.

Akiongea kwa niaba ya wazazi wa watoto waliopata msaada, Bi. Rosemary Chibwiga ameshukuru DUWASA na kumuahidi Mkuu wa Wilaya kuwa wazazi watajitahidi kuhimiza watoto wao kwenda shule pamoja na kuacha utoro na kwa pamoja wataacha tabia ya kuwashawishi Watoto kujifelisha kwani wametambua kuna watu wa kuwashika mkono.

Matangazo

  • Tangazo la nafasi ya kazi June 13, 2025
  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • TUSIFUMBIE MACHO MATUKIO YA UKATILI.

    June 16, 2025
  • DUWASA NA VEI WAKABIDHI MAHITAJI YA SHULE KWA WATOTO 105.

    June 13, 2025
  • DC. MAYEKA AFUNGA MAFUNZO YA UTHIBITI UBORA WA SHULE KATIKA WILAYA YA KONGWA

    June 02, 2025
  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.