• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Ekari 500 zatengwa kwa ajili ya uwekezaji Viwanda - Kongwa.

Imewekwa: July 2nd, 2022

Na Stephen Jackson, Kongwa.

Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Imetenga jumla ya Ekari 500 kwa ajili ya uwekezaji wa Viwanda.

Eneo hilo limetengwa katika kata ya Pandambili baada ya kuidhinishwa na wananchi kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika siku ya Jumamosi, Julai 2, 2022 ukihusisha wananchi, uongozi wa kata hiyo, Maafisa Ardhi na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Dkt. Omary Nkullo, ambaye alikuwa mgeni rasmi.

Katika Hotuba yake kwa Wananchi, ameeleza kuwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii "NSSF" umeomba kutengewa Ekari zipatazo 500 kwa ajili ya kujenga viwanda vya kuchuja mafuta ya Alizeti, viwanda vya sukari, nyanya, na uchakataji wa mazao ya mifugo.

Aidha ameongeza kuwa kuwepo kwa viwanda hivyo kutabadilisha taswira ya kata hiyo kutokana na ajira zitakazo zalishwa.

Wakati huo huo amewahakikishia wananchi kuwa licha ya eneo hilo kutengwa kwa ajili ya uwekezaji, wananchi wa kata hiyo wataendelea kuwa sehemu ya umiliki wa ardhi katika hati miliki itakayotolewa.

Wakizungumza kwa hisia, wananchi wamepongeza ujio wa mradi huo, wakiamini kuwa utakuwa ni sehemu ya suluhu ya tatizo la ukosefu wa ajira. ‘’Mradi tumeupokea. Tunapozungumzia kuupokea mradi ni kwamba haijalishi eneo litakuwa wapi, tuangalie hiyo fursa yenyewe iliyokuja ina uzito gani kwetu Pandambili’’ Alibainisha Daimoni Nuhu Masika, Mkazi wa Pandambili.

Naye Diwani wa kata, Mheshimiwa Onesmo S. Nyagwe, amemuomba Dkt. Nkullo, kufikisha Salamu za wananchi wa Pandabili kwa viongozi wa ngazi mbalimbali akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, kuwa Wananchi wamekubali kuupokea Mradi katika eneo lao.

Akihitimisha hotuba yake, Dkt. Nkullo amewashukuru wananchi na kuahidi kuwa mchakato wa upimaji wa eneo hilo unaanza mara moja ili kuwezesha upatikanaji wa hati miliki haraka iwezekanavyo.

Sanjali na hayo amewapongeza viongozi wa kata hiyo kwa kusimamia vizuri matumizi ya fedha za Tozo Tzs. Milioni  500 zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwaajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Pandambili, ambapo ameahidi kuwa serikali itawaletea madaktari pindi Ujenzi wa Kituo hicho Cha Afya utakapokamilika. ‘’Kitakapokamilika mapema na sisi tutajitahidi tuwaletee madaktari ili sasa upasuaji ufanyike papa hapa.’’ Alisema Dkt. Nkullo.

Ameongeza kuwa Eneo la Pandambili lipo kwenye mpango wa upimwaji ardhi Ili kuwezesha wananchi kumiliki ardhi kisheria.

Mkutano huo uliongozwa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Pandambili Ndugu Hussen Mohamed Ally ambaye alitoa shukrani za pekee kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri kwa ujio wake na habari njema kwa wananchi. 



Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.