• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Halmashauri ya wilaya ya Kongwa pamoja na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya yafanya kikao na Watendaji wa Kata na Vijiji.

Imewekwa: September 20th, 2024

Halmashauri ya wilaya ya Kongwa Pamoja na Ofisi ya Mkuu wa wilaya imefanya kikao kazi na watendaji wa Kata na Vijiji ili kuongelea mambo mbalimbali huku ajenda kuu ikiwa ni mapato. Baadhi ya mambo yaliyogusiwa ni Pamoja na changamoto kwa baadhi ya watendaji kuona kwamba jukumu la ukusanyaji wa mapato ni la timu ya mapato hivyo kutojihusisha ipasavyo.

Maeneo yaliyotiliwa msisitizo katika vyanzo vya mapato ni pamoja na ushuru wa madini ya ujenzi kama mawe, mchanga na kokoto, ushuru wa machinjio na ada ya ukaguzi wa nyama, ushuru wa magulio na minada, ushuru wa vibali vya mifugo, ushuru wa mazao, leseni za vileo na biashara nyingine pamoja na ushuru wa majengo.


Watendaji wa Kata na Vijiji wakiwa katika kikao katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa.

Akiongea na watendaji, Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka Simon Mayeka, amesisitiza umakini na uadilifu katika kusimamia mapato na amegusia Kata zenye madini kama Iduo, Chamkoroma na sehemu nyingine kuwa mstari wa mbele katika ukusanyaji wa mapato na usimamizi wa fedha za mapato maana hivyo ndio vyanzo vinavyoweza kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kukuza mapato ya Halmashauri.   

Aidha Mhe. Mayeka Simon mayeka amepata wasaa wa kuelezea kauli mbiu ya, ‘Kero yako wajibu wangu.’ Na kuwaasa watendaji kuwa falsafa hiyo inawataka watendaji kuhakikisha kwenye maeneo yao ya uongozi hakuna kero inayoachwa bila kutatuliwa kwasababu ni wajibu wao kuwahudumia wananchi kwa wakati.


Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka Simon Mayeka akiongea na Watendaji wa Kata na Vijiji.


Akihitimisha kikao, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa ndugu Fortunatus Mabula amewaasa watendaji wa Kata na Vijiji kufanya kazi kwa moyo wote kutumikia maeneo yao ya uongozi kwani ukusanyaji mzuri wa mapato utaunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan za kuboresha miundombinu na miradi mbalimbali ya maendeleo kutekelezwa kwa kasi katika Wilaya ya Kongwa.


Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa akiongea na Watendaji wa Kata na Vijiji.

Kikao hiki ni mahususi katika kuhakikisha watendaji wote wanaonyesha ushirikiano wa ukusanyaji mapato katika maeneo yao ya uongozi ili kuhakikisha Halmashauri inafanya vizuri zaidi katika eneo hilo. Ushirikiano huu ulichangia kupelekea Halmashauri kukusanya mapato na kufikia asilimia 92 ya bajeti ya mwaka wa fedha uliopita 2023/2024.

imeandaliwa na;

Mbonea E. Masha

Afisa Habari Wilaya ya Kongwa.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.