• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

IDARA YA MAENDELEO YA JAMII YAKABIDHI LISHE SHULE YA MSINGI VIGANGA.

Imewekwa: October 10th, 2024


Shule ya Msingi Viganga imekabidhiwa magunia mawili ya mahindi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa kwa ajili ya lishe. Idara ya Maendeleo ya Jamii ikiongozana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa imekabidhi lishe hiyo leo kwa uongozi wa shule Pamoja na jumuiya ya shule ya msingi Viganga.

Akiongea na wazazi waliojitokeza shuleni kwa ajili ya kushuhudia zoezi hilo, Afisa Maendeleo ya Jamii Ndg. Rahim Masengi ambaye amekuwa akiratibu usambazaji wa lishe mashuleni, amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa dkt. Omary Nkullo kwa kuona umuhimu wa elimu na wanafunzi kupata lishe shuleni sababu amekuwa akiendelea kutenga fedha ambazo zinatumika kununua nafaka ambazo husambazwa mashuleni.


Afisa Maendeleo ya Jamii, Ndg Rahim Masengi akiongea na wazazi.

Aidha ndg. Rahim Masengi, amesisitiza kuwa lishe hiyo inalenga wanafunzi wa umri mdogo ambao wapo chekechea na darasa la kwanza ambao kimsingi wazazi hawaonyeshi muamko mkubwa wa kuchangia lishe kwa ajili ya kundi hilo la wanafunzi.

Ndg Masengi ametoa wito kwa wazazi kuendelea kuchangia lishe shuleni sababu mchango mdogo wanaoutoa ni kwa ajili ya watoto wao ili kusudi waweze kupata elimu vizuri.

Akizungumza na wazazi wakati akikabidhi lishe, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Mhe. White Zuberi ameeleza wazazi kuwa huu ni wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Halmashauri zitenge asilimia moja ya mapato yake kwa ajili ya kuunga mkono wazazi kwa kununua lishe itakayosambazwa kwenye shule za msingi na sekondari.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Mhe White Zuberi akizungumza na Jumuiya ya Shule ya Msingi Viganga alipokuwa akikabidhi lishe.

Mhe White Zuberi amewaeleza wazazi kuwa waache mtazamo wa kulenga madarasa ya mitihani wanapochangia lishe bali wachangie lishe kwa madarasa mengine pia kwani hata wanafunzi wa madarasa ya chini ikiwemo chekechea wanahitaji kupata chakula wakiwa shuleni

Akiongea kwa niaba ya Jumuiya ya Shule ya Msingi Viganga, Mwalimu Mkuu ameshukuru uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa pamoja na Idara ya Maendeleo ya Jamii kwa kuunga mkono wazazi kwa kuwapatia lishe ili wanafunzi wapate chakula shuleni na kuongeza kuwa uungwaji mkono huo umekuwa faraja kubwa na Jumuiya ya Shule ya Msingi Viganga inashukuru.



Mpaka hivi leo magunia ishirini na sita ya lishe kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa yameshasambazwa kwenye shule ishirini na tatu zilizopo katika Kata mbalimbali za Halmashauri ya Kongwa ikiwa ni muendelezo wa kuunga mkono wazazi kwa kusambaza lishe mashuleni.

Imeandaliwa na;

Masha Mbonea

K/Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini (W)

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.