• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania azindua jengo la Mahakama ya Mwanzo Kibaigwa

Imewekwa: October 7th, 2021

  Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma, amezindua jengo la Mahakama ya Mwanzo katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Kibaigwa hii leo tarehe 07 Oktoba, 2021.

 Katika hotuba yake ya uzinduzi Mhe. Prof. Juma, amewashauri wananchi kutambua umuhimu wa usuluhishi baina ya wahusika wanaokabiliwa na migogoro ili kupunguza mashauri mahakamani na kuokoa muda jambo linaloweza kuongeza uzalishaji na kuboresha utoaji huduma kwa jamii.

Katika hotuba yake ameshauri kuwepo na chumba maalumu katika eneo la mahakama kwaajili ya wananchi kufuatilia Taarifa mbalimbali kwenye Tovuti kuhusu shughuli na huduma zitolewazo na Mahakama.

  Aidha Mhe. Jaji Mkuu, amewataka wananchi kuacha kubishana na viongozi wa mahakama au kulalamika pembeni kwa kuwa upo mfumo rasmi wa kuwasilisha malalamiko yao kila siku kupitia simu janja ambapo mlalamikaji hutakiwa kutuma ujumbe kuhusu malalamiko yake kwenye mfumo huo, nayo mahakama huyapokea na kuyashughulikia.

Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma, amewaasa pia wananchi kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano hasa simu janja ili kuendana na maisha ya karne ya 21.

  Jaji Mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma,  amesema hayo wakati alipokuwa akizungumza na wananchi na viongozi mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya mwanzo katika mamlaka ya mji mdogo wa Kibaigwa Wilayani Kongwa hii leo tarehe 07 Oktoba, 2021.

  Hotuba ya Mhe. Jaji Mkuu ilitanguliwa na hotuba ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jobu Yustino Ndugai ambaye alieleza kuwa kujengwa kwa mahakama hiyo ya mwanzo katika eneo hilo kutawapunguzia wananchi adha ya kusafiri umbali mrefu kufuata huduma. Mhe. Ndugai amewataka wananchi kuwaombea wafanyakazi wa Mahakama katika kazi yao ya utoaji haki, na kuhamasisha wahusika wote kuheshimu maamuzi ya mahakama ili haki iliyotolewa na mahakama itpatikane kwa wakati.

  Hafla hiyo ilihudhuriwa wananchi na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius Mwema Emanuel na kamati yake ya ulinzi na usalama ambapo alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, huku tukio hilo likipambwa na vikundi vya sanaa hasa ngoma na kwaya ya Mahakama.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.