Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Jeshi la Magereza Kongwa lapongezwa kwa Uhifadhi wa Mazingira

Imewekwa: January 27th, 2024

Na Stephen Jackson, Kongwa DC

Viongozi na Wananchi Wilayani Kongwa Wamelipongeza Jeshi la Magereza kwa jitihada za pekee za utunzaji wa Mazingira.

Katika kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 27 Januari, 2024 Katibu Tawala wa Wilaya ya Kongwa Bi. Sozi Ngate ameungana na wananchi na wataalamu kutoka taasisi mbalimbali kumtakia kheri ya kuzaliwa kwa kushiriki zoezi la ugawaji na upandaji miti, hafla iliyoandaliwa na Jeshi la Magereza Kongwa.

Katika Hotuba yake amepongeza jitihada za Mkuu wa Gereza hilo S.P. Tekla Ngilangwa na Jeshi la Magereza Kongwa kwa ujumla kwa bidii na maarifa ya kuotesha, kupanda,  kutunza miche ya miti na mingine kuigawa kwa wananchi kwa kuwa, siyo zoezi rahisi bali ni matokeo ya Jitihada binafsi za uongozi wa Gereza kwa kushirikiana na wadau wengine.

Bi. Sozi Ngate amewataka wananchi na taasisi zinazochukua miche hiyo kuipanda na kuitunza ili ikue na kuleta tija katika jamii. Aliongeza kuwa ni wajibu wa kila anayepanda Mti kuhakikisha mti unakua, hivyo ameelekeza kuwepo na taratibu maalumu wa usimamizi na  ufuatiliaji ili kila inayechukua mti ahakikishe unatunzwa huku wataalamu wakiendelea na utoaji wa elimu ya mazingira kwa jamii.

 "Elimu ya utunzaji wa mazingira ni muhimu sana sana" Alisema Ngate.

Akiwasilisha taatifa kwa Mgeni rasmi, SP. Tekla Ngilangwa, Mkuu wa Gereza Kongwa alisema, Jeshi la Magereza linaendesha mradi wa kitalu cha miche  kama darasa kwa wafungwa ili kuwawezesha kuwa wadau wa utunzaji wa mazingira pindi  wanaporejea kwenye jamii.

SP. Ngilangwa amesema kati ya Miche 100,000 iliyooteshwa kuanzia mwezi Agosti mwaka 2023, takribani miche 30,000 ilikufa kutokana na changamoto za hali ya hewa, ingawa jitihada za kuotesha Miche mingine  zinaendelea.

Jeshi la Magereza Kongwa linaendesha mradi wa kuotesha vitalu vya miche ya miti mchanganyiko kupitia mchango wa mfuko wa Misiti Tanzania (TaFF) na vyanzo vyake vya ndani  kisha kuigawa kwa taasisi mbalimbali na watu binafsi kama sehemu ya kuunga mkono jitihada za Serikali katika utunzaji wa Mazingira.

Naye Dkt. Omary NKullo, Mkurugenzi Mtebdaji (W) Kongwa alimshukuru Mkuu wa Gereza Kongwa S.P. Tekla Ngilangwa kwa kuandaa hafla ya ugawaji miti katika siku maalumu ya kusherehekea Siku ya kuzaliwa ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwahakikishia wananchi na watumishi kuwa zoezi linalofanyika la upandaji wa miti ni moja kati ya sadaka endelevu kwani matokeo ya miti hiyo yanalenga kunufaisha jamii na viumbe mbalimbali.

Kufuatia hafla hiyo, baadhi ya Watumishi na Wananchi wametoa pongezi kwa Jeshi la Magereza kwa mchango wao katika utunzaji na uhifadhi wa Mazingira na kuwatakia kheri kwa utaratibu huo mzuri wa ukarimu kwa jamii.

Kwa upande wake mwalimu Misayo Mtawa wa Shule ya Sekondari Mnyakongo ameeleza kufurahishwa na zoezi hilo na kuutaja uongozi wa Gereza hilo kuwa wa Ukarimu na mfano wa kuigwa, kwani kupitia zoezi hilo Wilaya ya Kongwa itazidi kuboresha mwonekano wa mazingira yake.

Naye Mwajabu Mbaruku Salum, ambaye ni Mlemavu wa Miguu, amemtaja Mkuu wa Gereza Kongwa S.P. Ngilangwa kama Kiongozi Mwanamke hodari wa Mabadiliko na mdau wa maendeleo kwa mba katika kipindi cha Uongozi wake amefanya mabadiliko makubwa katika gereza hilo ambayo hayakutarajiwa. " Ni mtoto mdogo lakini ana mawazo makubwa sana"  Alinukuliwa Mwajabu.

Aidha amewaasa watu wenye ulemavu kushiriki matukio ya kijamii kwani ulemavu siyo ugonjwa.

Matangazo

  • Tangazo la nafasi ya kazi June 13, 2025
  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.