• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

KAMATI MKTAKUWWA YAJA NA AZIMIO KUTOKOMEZA AJIRA ZA WATOTO

Imewekwa: August 18th, 2025

KAMATI MTAKUWWA YAJA NA AZIMIO KUTOKOMEZA AJIRA ZA WATOTO

Na Bernadetha Mwakilabi

Habari kongwa DC

Mwenyekiti wa kamati ya Mpango wa Taifa wa Kupambana na Ukatili wa Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka Simon Mayeka amemwagiza Afisa biashara kwa kushirikiana na Maafisa ustawi wa Jamii, pamoja na polisi kufanya msako wa sehemu za biashara zinazoajiri watoto ambao wana umri wa kuwepo shuleni na wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria ili kutokomeza Ajira za watoto katika Wilaya ya Kongwa. 

Azimio hilo limetolewa katika kikao cha kamati ya MTAKUWWA kilicholenga Kupokea, Kujadili na Kuidhinisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za MTAKUWWA kutoka katika Divisheni/Vitengo kwa kipindi cha robo ya Nne (Aprili- Juni, 2025) kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Mwenyekiti MTAKUWWA Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka S Mayeka akiongea na wadau katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Hospitali ya Wilaya Kongwa

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli za MTAKUWWA zilizofanywa na Divisheni ya Afya Ustawi wa Jamii na Lishe Bw. Deus Petro ameeleza kuwa Elimu ya Ukatili wa Kinjisia na ukatili dhidi ya Watoto imetolewa katika Kata ya Kongwa, Lenjulu, Kibaigwa, Ugogoni na Mlali ambapo huduma kwa wahanga wa ukatili wa Kijinsia na ukatili wa watoto wakiwemo wanawake 331 na Watoto 10 waliofanyiwa ukatili walipatiwa huduma na kuongeza kuwa kesi 8 zimefanyiwa mchepuo na Kesi 2 zimefikishwa mahakani kwa uamuzi zaidi.

Bw. Deus ameongeza kuwa jumla ya Watoto 45 wanaishi kwenye mazingira hatarishi wametambuliwa na jumla ya Watoto 12 wakiume wanaoishi katika mazingira hatarishi na kufanya kazi mtaani wametambuliwa na kuunganishwa na familia zao huku watoto 2 wakike waliokuwa wameajiriwa kufanya kazi za ndani katika umri mdogo wameokolewa na kuunganishwa na familia zao za awali.

Akiwasilisha taarifa ya shughuli za MTAKUWWA zilizofanywa na Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Bw. Allen Msumule ameeleza kuwa Divisheni imeratibu na kufanya ufuatiliaji wa vikundi vya Malezi 68 ambavyo wajumbe wake ni wanawake wenye watoto chini ya miaka mitano na wanawake wajawazito ambapo Wazazi/walezi   waliopata elimu kuhusu malezi Chanya ni 1,078.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Huduma za sheria, Bi. Hella Mlimanazi ameeleza kuwa kitengo kimechukua hatua za kuandaa mikataba yenye lengo la kuwataka wazazi kuhakikisha watoto wao wanahudhuria shule kikamilifu na kuwa na ufaulu unaoridhisha na kutowaachisha masomo yao ili kuwapeleka kufanya shughuli zingine kinyume na sheria, jambo linalopelekea watoto kufanyiwa ukatili wa kijinsia kwa tamaa za wazazi wao za kujipatia fedha kupitia kazi wanazofanyishwa watoto.

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kazini September 23, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili September 02, 2025
  • Tangazo la nafasi ya kazi June 13, 2025
  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • JAMII IMETAKIWA KUTAMBUA HAZI ZA MNYAMAKAZI PUNDA

    September 26, 2025
  • RC SENYAMULE AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MADARASA SHULE YA MSINGI KONGWA

    September 25, 2025
  • KITUO CHA AFYA KUJENGWA KATA YA SAGARA

    September 22, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII AJIRA MPYA WALA KIAPO

    September 19, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.