• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Kamati ya Fedha yasisitiza matumizi mazuri ya fedha

Imewekwa: November 23rd, 2023

Na Stephen Jackson, Kongwa DC

Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango Wilayani Kongwa imewataka wataalamu wa Halmashauri kutumia vizuri fedha zinazotolewa na Serikali kukamilisha miradi mbalimbali ya kimkakati badala ya kutegemea fedha za mapato ya ndani kukamilisha Ili fedha hizo zitumike kutatua changamoto zinazoikabili Jamii.

Kamati imetoa Maelekezo hayo Novemba 23, 2023 kwenye kikao chake baada ya Mhe. Job Yustino  Ndugai Mbunge wa Jimbo la Kongwa na Spika mstaafu wa Bunge Kuhoji sababu za kutokamilisha miradi Kwa fedha zinazotolewa na serikali, hoja iliyoungwa mkono na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. White Zuberi Mwanzalila.

Aidha Mhe. Ndugai amesisitiza Divisheni ya Mipango na Uratibu kuelekeza matumizi ya fedha kwenye Mipango ya Halmashauri iliyoidhinishwa na Menejimenti.

Katika hatua nyingine, Mhe. Ndugai amekemea matumizi ya Magari ya Halmashauri yasiyozingatia Maslahi ya umma na kuitaka Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu kusimamia vizuri usalama wa Madereva pamoja na Magari.

Akiwasilisha taarifa ya mapato na Matumizi kwa kipindi cha Mwezi Oktoba, 2023  Ndugu Mark Vicent Kahogo kwa niaba ya Mkuu wa Kitengo cha Fedha CPA. Deodatus Mutalemwa alisema Halmashauri ilifanikiwa kukusanya jumla ya Shilingi 248,464,175.86 kutoka vyanzo vya mapato ya ndani visivyolindwa.

Naye Mtaalamu wa Uchumi kutoka Divisheni ya Mipango na uratibu, Bwana Erasto Unambwe alitoa Mapendekezo ya miradi inayohitaji kuidhinishiwa fedha kwa mujibu wa bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 yenye jumla ya Shilingi 99,299,670.34 ikihusisha mradi wa upimaji viwanja katika eneo la njia panda ya kuelekea Mpwapwa, mapendekezo ambayo kamati ya fedha haikuidhinisha kutokana na kutokuwepo kwa mchanganuo wa matumizi ya fedha na badala yake kamati imeelekeza taarifa hiyo irekebishwe na kuwasilishwa tena katika kikao kijacho.

Akichangia taarifa hiyo Diwani wa Kata ya Mkoka na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Richard Mwite amepinga pendekezo la kupima viwanja katika eneo hilo badala yake amependekeza fedha hizo zielekezwe kwenye eneo la Mkoka ambalo lilipimwa takribani miaka 6 iliyopita na hadi Sasa mchakato wa umilikishaji viwanja haujakamilika.

Naye Diwani wa Kata ya Sejeli Mhe. Chilingo Chimeledya amesema pamoja na pendekezo la kuboresha Mazingira ya baadhi ya minada hususani mnada wa Matanga, pia Machinjio ya Mnada wa Mbande iboreshwe Kwa kuwa Mazingira yake si rafiki kwa Afya za walaji wa nyama.

Chimeledya ameongeza kuwa DUWASA inaendelea na mchakato wa kutatua changamoto ya Maji katika kijiji Cha Mbande Kwa kusambaza Maji umbali wa Kilometa 4 na amependekeza usambazaji huo uguse pia eneo lililopimwa viwanja hivi karibuni Ili kuboresha eneo hilo na kuvutia uendelezaji.

Akihitimisha hoja ya Mapendekezo hayo, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. White Zuberi Mwanzalila ameitaka Divisheni ya Mipango na Uratibu kurekebisha taarifa hiyo ikihusisha mchanganuo wa kila pendekezo na kuiwasilisha katika kikao kijacho Ili iweze kujadiliwa na kupata ridhaa ya Wajumbe sambamba na kuipongeza Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi Kwa kuongeza ufaulu katika matokeo ya Darasa la Saba yaliyotangazwa na baraza la mitihani la taifa Nov. 23, 2023.


Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.