• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Kamati ya Ushauri yaridhika na Utekelezaji wa Mradi wa kuhimili mabadiliko ya Tabianchi

Imewekwa: September 16th, 2022

Na Stephen Jackson, Kongwa.

Kamati ya Ushauri ya mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi unaotekelezwa Wilayani Kongwa na Shirika lisilo la kiserikali la "Foundation for Energy, Climate and Environment (FECE) imeridhishwa na hatua ya Utekelezaji wa miradi kwa awamu ya kwanza.

Akizungumza kwa niaba ya Kamati Septemba 16, 2022,  Mwenyekiti wa kamati hiyo Ndugu Stephen Mariki amesema kuwa katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mradi, jumla ya Dola za kimalekani laki nne (400,000) zimetumika na kamati imejiridhisha kuwa miradi imetekelezwa kama ilivyokuwa imepangwa.

Wajumbe wa kamati ya ushauri mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi wakiwa kwenye kikao, ukumbi wa biashara Kongwa Tarehe 16 Septemba, 2022.

Ndugu Mariki ameongeza kuwa katika kipindi cha miaka miwili iliyosalia, shughuli zitaongezeka sambamba na ongezeko la bajeti ambapo kwa mwaka wa pili jumla ya Dola za kimalekani 455,927.36 zimepangwa kutumika.

Kwa dhumuni la kuhakikisha Malengo ya mradi ya kuwajengea uwezo wakulima na wafugaji kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, kamati imelishauri shirika la FECE kuwashirikisha kikamilifu wataalamu katika usimamizi wa miradi kwa minajiri ya kuongeza tija.

Katika picha ni Mwenyekiti wa kamati Ndugu Stephen Mariki kutoka Shirika la FECE akiwa pamoja na Ndugu Godfrey Mujairi ambaye ni mtaalamu wa Mazingira kutoka Halmashauri.

Akichangia hoja hiyo, mjumbe wa kamati Ndugu Juma Selemani kutoka Shirika la FECE, amewataka wataalamu wanaohusika na miradi inayotekelezwa kutoa ushirikiano wa kutosha ili kufanikisha miradi kupitia bajeti zilizotengwa.

Ndugu Juma Selemani msimamizi wa mradi kutoka Shirika la FECE.

Naye Mwenyekiti mweza wa kamati hiyo Mhe. White Zuberi Mwanzalila licha ya kuwashukuru wajumbe wa kamati kwa kufanya ziara ya kutembelea miradi pia amewasisitiza wasimamizi kuhakikisha miradi inayotekelezwa inazingatia viwango vya serikali.

Awali kamati hiyo ilitembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa katika Kata mbili za Ugogoni na Mtanana, ambapo wajumbe walijionea hali halisi na kutoa Ushauri na Mapendekezo yao.

Wajumbe wa kamati wakiwa kwenye mradi wa umwagiliaji wa bustani kwa njia ya matone katika Shule ya msingi Ndalibo.

Miongoni mwa Miradi iliyotembelewa ni pamoja na ujenzi wa Majosho na malambo ya kunyweshea mifugo, miundombinu ya maji, usitawishaji wa miti, pamoja na kilimo cha umwagiliaji.

Nao walimu wakuu wa shule za msingi za Mtanana na Ndalibo, kwa nyakati tofauti wameelezea hali ilivyo katika miradi iliyopo kwenye maeneo yao.

Mwalimu Musa Abeli Mkatalo wa Shule ya msingi Mtanana alidai kuwa jumla ya miche 1000 ya  mikorosho ilipokelewa mwanzoni mwa mwezi Machi na kupandwa na wanafunzi lakini kutokana na changamoto ya upatikanaji wa maji, na ufugaji holela, baadhi ya miche ilikufa.

Miche ya mikorosho katika Shule ya msingi Mtanana wakati wa ukaguzi. Picha na Stephen Jackson.

Naye Mwalimu mkuu wa Shule ya msingi Ndalibo  Bwana Nyanje Nyanje, amedai kuwa kuwepo kwa mradi wa kisasa wa umwagiliaji wa bustani, kumekuwa ni neema kwa wanafunzi na wananchi kwa kuwa unatumika kama shamba darasa,  na kwamba mradi utasaidia kupunguza kiasi fulani cha changamoto za lishe.

Miradi huu unasimamiwa na Kamati hiyo inaundwa na wajumbe kutoka kutoka Shirika la FECE, Halmashauri , wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo, RUWASA, TFS Kongwa, NEMC, na DUWASA.

 

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.