• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Wafugaji watakiwa kuvisha hereni za Kielektroniki mifugo yao.

Imewekwa: September 19th, 2022

Na Stephen Jackson, Kongwa.

Afisa Mifugo Wilayani Kongwa Bwana Msafiri Vedastus Mkunda, amewataka wafugaji Wilayani hapa kuchangamkia zoezi la uvishaji wa hereni za Kielektroniki mifugo yao ili itambulike kimataifa.

Akizungumza na wafugaji wakati wa ukaguzi wa mchakato wa zoezi, Mkunda amesema wafugaji wanatakiwa kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan za kuwatafutia masoko.

Amesema katika soko la kimataifa, kwa kutumua alama (bar code) iliyochapishwa kwenye hereni iliyovishwa, Mdau wa mifugo anaweza kutambua nchi, mkoa na wilaya na hata kata ambapo mifugo inatokea.

Ameongeza kuwa, hereni hizo za Kielektroniki zinasaidia usalama wa mifugo kwa kuzuia wizi na kuthibiti kuenea kwa magonjwa kabla ya kusambaa, na pia kuwawezesha kuikatia bima mifugo yao kwa ajili ya kudai fidia pindi mifugo inapokumbwa na Majanga.

Kwa mujibu wa Afisa Mifugo Mkunda, Zoezi la kuvisha hereni lilipangwa kuanzia Mwezi Aprili, 2022 na kukamilika ifikapo mwishoni mwa mwezi Septemba na baada ya hapo mfugaji ambaye mifugo yake haitakuwa imevishwa hereni hatua za kusheria zitachukuliwa dhidi yake ambapo anaweza kutozwa faini isiyozidi shilingi milioni mbili, kifungo cha miezi 6-12 au vyote kwa pamoja na kuanzia Novemba 1, 2022 mifugo isiyo na hereni haitaruhusiwa ndani ya minada ya Halmashauri ya Kongwa.

"Kuanzia tarehe 1 mwezi wa 11 kwa utaratibu ambao tumejiwekea kwa wilaya yetu huyo mfugaji hatoruhusiwa kabisa kuuza mifugo yake ndani ya minada yetu rasmi" alisema Mkunda.

Aidha lengo la Wilaya ni kuvisha hereni mifugo ipatayo165,379 ikihusisha ng'ombe, mbuzi, kondoo n.k lakini mpaka sasa jumla ya mifugo 14,386 imevishwa.

Kwa upande wao wafugaji wameilalamikia serikali kuwatoza kiasi cha shilingi 1750 kwa kila ngo'mbe au punda mmoja na shilingi 1000 kwa kila mbuzi au kondoo mmoja.

Bi. Rabia Msofe ambaye ni mfugaji  kutoka Kongwa, licha ya kuunga mkono makalamimo kuhudu changamoto ya gharama, ameipongeza serikali kwa zoezi hili la kidigitali na kuiomba Serikali kujenga majosho ya kuogeshea mifugo ili kuthibiti magonjwa ya mifugo.

Kwa upande mwingine, Bwana Daud Ramadhan Masoud ambaye ni mfugaji wa kata ya Kongwa ameiomba Serikali kupunguza gharama ili kuwawezesha kumudu garama za zoezi hilo, malisho na madawa kwa ajili ya mifugo yao

Zoezi la uvishaji wa hereni za Kielektroniki ni mwendelezo wa jitihada za serikali za tangu mwaka 2015 ambapo serikali iliagiza utiaji chapa kwa mifugo kwa njia za asili, na sasa teknilijia mpya ya hereni inahamasishwa kwani mifugo inaweza jutambulika kirahisi mahali inapotokea ikihusisha nchi, Mkoa, Wilaya na Kata.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.