• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Baraza la Madiwani Kongwa Laomba Katibu Mkuu Utumishi Kurejea Kauli Yake

Imewekwa: May 25th, 2018

Katika Mkutano wa Baraza la Madiwani tarehe 24 Mei, 2018, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Mhe. White Zuberi amemuomba Katibu Mkuu Utumishi kurejea kauli ya kwamba, "Mkurugenzi hana ruhusa ya kumzuia uhamisho wa mtumishi pindi anapotaka kuhama".

Katibu Mkuu Utumishi ameombwa kufuta kauli hiyo kufuatia changamoto kubwa ya kuhama kwa idadi kubwa ya watumishi kwa kipindi ambacho Halmashauri ya Kongwa inakabiliwa na upungufu mkubwa wa watumishi wa Idara mbalimbali hususani Idara za Elimu na Afya.

Mhe. White amesema Katibu Mkuu Utumishi alitoa kauli hiyo Katika Mkutano Rasmi uliyojumuisha Wenyeviti wa Halmashauri, Maafisa Utumishi, Wakurugezi, Maafisa Mipango, na Mameya wote.

Mhe. White anaeleza kwamba licha ya aadhi ya watumishi kupungua kwa kutolewa kutokana na kukutwa na vyeti vya kugushi (fake) wakati wa Zoezi la Uhakiki wa Watumishi Hewa, kwa Kipindi cha miezi mitatu Watumishi 73 wamehama,  baada ya kauli ya Katibu Mkuu Utumishi.

Alisisitiza kwamba Kauli hiyo ya Katibu Mkuu Haitendi haki kwa Halmashauri ya Kongwa na zingine Nchini kote hasa zilizopo pembezoni na hali inayoleta hofu ya maeneo yaliyopo pembezoni Kukosa wafanyakazi kwani watakuwa wakihama kuhamia mjini na kukwepa maeneo ya vijiji vya Pembezoni.

Kadhalika ameeleza kuna baadhi ya maeneo watumishi walikuwa wakigoma kwenda, lakini Halmashauri ilikuwa ikiwapa motisha ili waweze kuvumilia kuishi, hivyo, tafsiri ya kauli hiyo ya Katibu Mkuu inasababisha watumishi wengi waliopo maeneo yenye Changamoto kuhamia mjini na kuendelea kuongeza Tatizo la upungufu wa watumishi.

Hivyo, Katibu Mkuu anapaswa Kutengua  Kauli hiyo, na suala la uhamisho aliomba aachiwe Mkurugenzi kuhamisha watumishi wenye sababu ya msingi tu, kwani haitakuwa busara kuomba watumishi kupitia Bajeti, Halafu wahame kiholela, pia utendaji wa huduma kwa wananchi utapungua Sana na Kusabisha lawama kwa Serikali.

Aidha, alisema Tayari Serikali imeshaleta idadi ya watumishi watakaoajiriwa Mwaka wa Fedha 2018/19 ambapo Halmashauri ya Kongwa imepitisha nafasi 600 za ajira, lakini Kauli hiyo Kama itaendelea kutumika basi hata wakiajiriwa watumishi wengi bado wataendelea kuhama na ukubwa wa Tatizo kubaki pale pale.

Madiwani kutoka Kata Mbalimbali za Halmashauri ya Kongwa kwa pamoja wameunga mkono  Hoja hii na baadhi yao wanasema wana matumaini Katibu Mkuu ataridhia na hatimaye Kufuta kauli hiyo.

Diwani wa Kata ya Mlali, Mhe Richard Mngurumi ameeleza kwamba Zahanati ya Ihanda katika Kata yake imefungwa baada ya mtumishi aliyekuwapo kuhama, licha ya mtumishi mmoja kuondolewa kutokana na sakata la vyeti vya kugushi.



Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.