• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Serikali ya Namibia yawapa faraja Akinamama waliopoteza watoto wao baada ya wapigania Uhuru.

Imewekwa: March 2nd, 2022

Na Stephen Jackson, Kongwa.

Naibu waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Nchini Namibia Mhe. Jennelly Matundu , Leo Tarehe 2 Machi, 2022 , Amefanya ziara Wilayani Kongwa.

Katika ziara hiyo amekutana na Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius Mwema Emmanuel na kufanya mazungumzo na akinamama  kadhaa wanaodai kupoteza watoto wao miaka kadhaa iliyopita.

Inadaiwa kuwa Watoto hao walichukuliwa na kupelekwa nchini Namibia kwa lengo la kupelekwa shule na hawakuweza kurejeshwa hadi sasa.

Wakielezea kwa masikitiko, akina mama hao walieleza kuwa wamepoteza matumaini ya kuwapata watoto wao kwani hawana mawasiliano nao kwa muda mrefu, hivyo wameiomba serikali ya Namibia kufuatilia Jambo hilo.

Akizungumza kwa masikitiko, Mara baada ya kupokea maelezo hayo, Mhe. Jennelly Matundu, amesema kuwa maelezo hayo yanaamsha simanzi, hivyo ameahidi kuwa serikali ya nchi yake itayafanyia kazi na familia  hizo zitapatiwa mrejesho kupitia ubalozi wa Namibia Nchini hapa.

Baada ya mazungumzo hayo ya muda mrefu, Naibu huyo wa wizara ya mambo ya nje ya Namibia, ametembelea katika makumbusho ya iliyokuwa kambi ya Wapigania Uhuru ambayo kawa sasa ni Shule ya Sekondari Kongwa, ambapo alipokelewa na uongozi wa shule hiyo Kisha kuongea na wanafunzi  na kuhitimisha ziara hiyo kwa kutembelea Makaburi ya Mashujaa wa Namibia yaliyopo kitongoji cha Morisheni mjini Kongwa.

Mambo mengine yaliyozungumziwa ni pamoja na mpango wa kuboresha miundombinu katika maeneo hayo ya kihistoria ili kuwa moja ya sehemu zitakazovutia watalii.

Mhe. Matundu alifuatana na Balozi wa nchi hiyo hapa nchini Mhe. Lebbius Tangeni Tobias na Maafisa wengine kutoka Namibia ambapo Kamati kuu ya ulinzi na Usalama ya Wilaya,  ya Kongwa, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. White Zuberi Mwanzalila, viongozi wa CCM (W), kaimu Mkurugenzi Mtendaji (W) na baadhi ya Maofisa kutoka Halmashauri ya Kongwa walihudhuria.


Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.