• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

KONGWA KUENDELEA KUTEKELEZA MKAKATI WA LISHE SHULENI.

Imewekwa: February 5th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa inaendelea kujikita katika uboreshaji wa  mkakati wa utoaji lishe katika shule za msingi na sekondari ilikuchochea matokeo mazuri ya wanafunzi Pamoja na kuongeza mahudhurio ya wanafunzi shuleni.

Hayo yameelezwa na Afisa elimu msingi Wilaya ya Kongwa bi Margreth Temu alipokuwa akitoa taarifa ya lishe shuleni ambapo amesema kuwa asilimia 100 ya shule za msingi Wilayani Kongwa, wanafunzi wake wanakula chakula shuleni.

Aidha Mwl. Magreth Temu amefafanua kuwa kumekuwa na changamoto ya upatikanaji wa maji hali inayopelekea kukwamisha upandaji wa miti ya matunda ambapo upandwaji miti ya matunda kwa wingi ungeongeza tija katika swala la lishe shuleni kwani wanafunzi wangepata matunda katika chakula wanachopata shuleni ili kuongeza virutubisho katika ukuaji wao. Bi Magreth ameongeza kuwa kila shule imeunda klabu ya mazingira ili kusimamia suala la usafi wa mazingira na upandaji miti kwa wingi Pamoja na kutunza vyanzo vya maji.

 Kwa upande wake Afisa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Wilaya ya Kongwa Bwana Msafiri Mkunda ameeleza kuwa katika robo ya pili ya Oktoba/Desemba 2024, Idara imeweza kuandaa mashamba darasa kwa shule za sekondari na msingi 172 na kusambaza tani 7 za mtama utakaopandwa katika mashamba hayo ili kusudi mavuno yatumike kama chakula shuleni. Ameongeza kuwa uamuzi wa kuchagua mbegu za mtama ni wa kisayansi kwani mbegu hizo zinaweza kukabiliana na hali ya ukame hivyo kusaidia kuwepo kwa mavuno baada ya msimu wa kulima kuisha.

Nae Afisa lishe Wilaya ya Kongwa Bi. Maria Haule amesema wamefanikiwa kuongeza idadi ya wanafunzi wanaokula shuleni kutoka 83% kwa kipindi cha July-Sept 2024 hadi 90.2% kwa kipindi cha Oktoba-Disemba 2024 na dhumuni ni kuhakikisha kuwa wanafunzi asilimia mia moja wanapata chakula Shuleni kama jinsi malengo yanavyoelekeza.

Nae mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Dkt Omary Nkullo amesema taarifa ya lishe itolewe mapema na mara kwa mara ili kusaidia utekelezaji na utatuzi wa changamoto zinazojitokeza katika kutekeleza mkakati wa kuhakikisha wanafunzi asilimia mia moja wanapata chakula shuleni.

Akifunga kikao hicho mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mheshimiwa Mayeka Simon Mayeka amewataka Watendaji wa Vijiji na kata kufanya kazi kwa ufanisi ili matokeo ya kazi zao yaonekane katika jamii "uongozi ni matokeo tusipike taarifa" na suala la chakula shuleni ni mkataba wa lazima.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.