• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Kongwa kumalizia tatizo la Upimaji Ardhi.

Imewekwa: February 14th, 2023

Na Stephen Jackson, Kongwa DC

Kununuliwa kwa vifaa vya kisasa vya Upimaji wa Ardhi Wilayani Kongwa kutapelekea mapinduzi makubwa ya utatuzi wa changamoto mbalimbali zilizokuwa zikiwakabili wananchi ikiwemo ujenzi holela.

Serikali kupitia Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya makazi, imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali kutatua migogoro ya Ardhi kote Nchini na kuhamasisha wananchi kuchangamkia fursa za kumilikishwa Ardhi na kuiendeleza sanjali na kujipuesha na ujenzi holela.

Makampuni kadhaa yamekuwa yakishirikiana na Serikali kurasmisha maeneo ya makazi na kupima Ardhi kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma za jamii. Hata hivyo changamoto kubwa imekuwa ni uwezo hafifu wa baadhi ya Halmashauri wa kutokuwa na vifaa vya Uhakika vya Upimaji Ardhi.

Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa imejizatiti kuhakikisha tatizo la ujenzi holela linakuwa Historia, na ndiyo sababu ilifanya maamuzi magumu ya kununua vifaa vya kisasa kwa ajili ya kupima Ardhi ambavyo tayari vimewasili na kufanyiwa majaribio ambayo yalitoa matokeo chanya.

Katika baraza la Madiwani la tarehe 10 Februari 2023,  Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Dkt. Omary A. Nkullo aliwaeleza wajumbe kuwa Divisheni ya Ardhi imefanikiwa kununua vifaa vya kisasa vya kupima Ardhi ambavyo vina uwezo mkubwa kuliko makadirio ya awali.

Alisema Kifaa hicho kinachoitwa RTK kilichonunuliwa ni cha kisasa Sana chenye uwezo wa kupima umbali wa km 20 na Hivyo baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa linaandika rekodi ya kuwa miongoni mwa Halmashauri chache zenye vifaa vya kisasa vya Upimaji Ardhi.

"Wakati tunapata specifications, tuliandika km. 8 kwenye specifications lakini yule bwana ametuletea yenye km. 20" - Dkt. Nkullo.

Ameongeza kuwa awali Halmashauri ilikuwa ikikodishwa kifaa Cha Upimaji kwa thamani ya shilingi 300,000.00 kwa Siku, Sasa endapo baraza litaridhia kifaa hicho pamoja na kutumiwa na Divisheni ya Ardhi pia kinaweza kukodishwa maeneo mengine na kuwa sehemu ya vyanzo vya mapato ya ndani.

Kwa hali hii kuna Kila sababu ya kuupongeza uongozi mzima wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa kuanzia mwenyekiti wake Mhe. White Zuberi Mwanzalila, Makamu wake Mhe. Richard Mwite, Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri Wilaya ya Kongwa Dkt.Omary A. Nkullo, waheshimiwa Madiwani wa Kata zote 22 za Wilaya ya Kongwa na Kamati zote za Madiwani pamoja na wakuu wa Divisheni, vitengo na Seksheni.

Kila jambo hutegemea zaidi uthubutu ndipo liweze kufanikiwa. Ni lazima jitihada hizi za kubuni namna ya kutatua changamoto kwa kubaini vipaumbele zitiliwe mkazo Kwa kila changamoto ndipo mafanikio yatakapofikiwa.

Dkt. Nkullo alisisitiza kwamba seti ya vifaa hivyo vya kisasa (RTK) ni yenye thamani kubwa ingawa hakuitaja amesema ni lazima vitunzwe kwa umakini na uangalizi mkubwa Ili viweze kudumu na Hivyo kuleta tija kwa manufaa ya umma.

Wajumbe wa baraza la Madiwani, walipiga makofi ishara ya kushangilia mafanikio ya Halmashauri, kinachosuburiwa Sasa ni matokeo ya utatuzi wa changamoto za ardhi. Kufikia azma hiyo itawalazimu watumishi wa Divisheni hiyo kujituma kwa kila hali Ili kuleta tija iliyokusudiwa.

Matangazo

  • Kuitwa kwenye Usaili Ajira za muda -TASAF December 02, 2022
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2022 December 01, 2022
  • Kuitwa kazini Ajira za Muda - TASAF December 06, 2022
  • Fomu ya Maelekezo ya kujiunga na shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa. May 18, 2022
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • Viongozi wa kisasa watakiwa kushirikiana na wataalamu

    March 12, 2023
  • Watendaji wote waahidiwa kupewa pikipiki

    February 17, 2023
  • Kongwa kumalizia tatizo la Upimaji Ardhi.

    February 14, 2023
  • Mkurugenzi Kongwa aonya wazazi wanaokatisha tamaa wanafunzi.

    February 13, 2023
  • Tazama Yote

Video

''KONGWA MMEUPIGA MWINGI''
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)
  • Bunge la Tanzania

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 737 798 222

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.