• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Kongwa yaanza kutekeleza Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi

Imewekwa: October 12th, 2021

Na Stephen Jackson na Nkinde , Kongwa.

Halmashauri ya wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma inatekeleza mradi wa mazingira ili kuiwezesha kuhimili mabadiliko ya tabianchi.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Mhe. Dkt. Samwel G. Mafwenga wakati alipokuwa akihutubia katika Mkutano wa uzinduzi wa mradi wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi kwa jamii za wakulima na wafugaji wilayani Kongwa tarehe 12, Oktoba 2021 katika ukumbi wa chuo cha VETA wilayani Kongwa.

Katika hotuba yake pia alieleza kuwa mwishoni mwa Mwaka 2017 taasisi anayoisimami (NEMC) ilipata ithibati ya kuwa wakala wa taifa wa mfuko wa kimataifa wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi. Kufuatia hatua hiyo ya kuthibitishwa na kuwa mwangalizi wa miradi ya mazingira, Shirika la Foundation for Energy Climate and Environment (FECE), kwa kushirikiana na Halmashauri ya Kongwa waliandika andiko la mradi lililokubalika kimataifa na kuwa miongoni mwa maandiko manne (4) yaliyoidhinishwa kati ya maandiko mia moja na sita (106) yaliyowasilishwa.

Aidha Dkt. Mafwenga ameelezea kufarijika na kazi aliyoifanya Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mbunge wa jimbo la Kongwa Mhe. Job Yustino Ndugai kwa jitihada zake zilizopelekea kufanikiwa kwa mradi huo wenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni  moja na laki mbili sawa na Tzs. Bilioni 2.7.

Kwa upande wake Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Y. Ndugai (Mb) ameshukuru sana kutolewa kwa Fedha hizo kwani zitasaidia kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Mhe. Ndugai Ametumia fursa hiyo kuwasisitiza viongozi wa vijiji ambavyo mradi huo unatekelezwa, kuupokea kwa mikono miwili kwa kuwa mradi huo ni mzuri kwani utahusisha usambazaji wa maji, na pia miradi ya kilimo cha mazao mbalimbali kama vile mtama, ufuta viazi vitamu n.k na pia utawezesha utoaji wa mafunzo mbalimbali.

Akitolea ufafanuzi kuhusu mradi huo, Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Foundation for energy climate and Environment (FECE) Dkt. Dominico Klemo ameeleza kuwa mradi huu wa miaka mitatu utatekelezwa na shirika hilo  kwa kushirikiana na wilaya ya Kongwa chini ya uangalizi wa NEMC lengo likiwa ni kuzinufaisha Kata mbili za Ugogoni na Mtanana.

Mradi huu wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi unalenga kusaidia upatikanaji wa maji ya uhakika kwa wakazi wa kata husika, Kuwezesha shughuli za wananchi kuwa endelevu, kutunza mazingira ili yaweze kuwalinda wananchi dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na kujenga uwezo wa taasisi na maafisa katika wilaya ya Kongwa juu ya namna bora ya kukabiliana na Majanga yanayoweza kujitokeza.

Akihitimisha Mkutano huo wa uzinduzi wa mradi, Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius Mwema Emanuel amewataka wasimamizi wa mradi huo kuwa wazalendo ili malengo ya mradi huo yaweze kutimia.

Mradi huu umezinduliwa rasmi na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai mbele ya Mkuu wa wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius Mwema Emanuel na viongozi mbalimbali na wadau wa mazingira wilayani Kongwa.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.