• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Kongwa Yafanya Mkutano wa Pamoja; Baraza la Biashara la Wilaya, Baraza la Madiwani

Imewekwa: December 20th, 2017

Wilaya ya Kongwa yafanya Mkutano wa Pamoja wa Baraza la Biashara la Wilaya na Baraza la Madiwani Wilayani Kongwa. Katika Mkutano huu Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Deogratius Ndejembi (Mwenyekiti wa Baraza la Biashara) amewahasa wajumbe wa mabaraza yote mawili -sekta ya umma na sekta binafsi kujikita kwenye mradi wa ufugaji kuku. 

Aidha, Mkuu wa Wilaya ameeleza elimu ambayo wataalam wanayo na wadau mbalimbali wa biashara waliyopewa kuhusu ufugaji kuku washirikiane katika kuisambaza kwa wananchi katika kata zote zilizopo Wialayani kongwa. Hayo ameeleza wakati wa kufunga Mkutano huo ambaomumefanyika tarehe 20 Desemaba, 2017.

Katika Mkutano huo mada mbalimbali zimewasilishwa na kujadiliwa ikiwemo; Mafanikio ya na Changamoto za Baraza la Biashara la Wilaya kwa mwaka 2017; Uanzishaji wa Dira ya uwekezaji kwa Wilaya ya Kongwa' na Taarifa ya Utekelezaji wa Mradi wa Kuku Mbande.

Katika taarifa ya mafanikio na changamoto imeelezwa kwamba Baraza la Biashara kwa mwaka 2017 limepata mafanikio yafuatayo;

  • Kuundwa kwa Baraza jipya la Biashara lenye uwakilishi mpana zaidi na lenye kujumuisha jumuiya mbalimbali;
  • Vikao mbalimbali vya Baraza la Biashara vimefanyika pamoja na vikao vya kamati tendaji. Vikao vya Baraza la Biashara la Wilaya- 3, vikao vya kamati tenda- 4, vikosi kazi- 3, Baraza la pamoja kati ya Baraza la Biashara na Baraza la Madiwani- 1;
  • Vikosi kazi vimeundwa kubaini fursa na changamoto za Soko la mazao Kibaigwa, na kikosi kazi cha kubaini changamoto za Soko la mifugo Kongwa;
  • Kuanza kwa utekelezaji wa mradi wa kuku katika eneo la Mbande na kiasi cha Tsh.115, 092,500/= zimeshatolewa kwa awamu ya kwanza;
  • Mafunzo ya kujengewa uwezo yametolewa kwa wajumbe wa Baraza la Biashara kutoka Sekta binafsi yametolewa kwa kushirikiana na TPSF;
  • Kuundwa kwa kikundi cha umoja wa wauza mafuta ya alizeti Pandambili- UVIWAPA ukijumuisha muunganiko wa vikundi nane;
  • Maandiko mbalimbali ya miradi yameandikwa na kuwasilishwa LIC ikiwemo andiko la mradi wa kituo cha kuuzia mafuta ya alizeti Pandambili na andiko la mnada wa mifugo Mbande; na
  • Kuanza kutumia jengo la Biashara, na hadi sasa kituo hicho kimeweza kutoa huduma mbalimbali na kuweza kusajili wafanyabiashara 706.

Kuhusu Uanzishaji wa Dira ya uwekezaji kwa Wilaya ya Kongwa, imeelezwa kwamba Dira hiyo itatumika kama chanzo cha habari za uwekezaji katika Wilaya ya Kongwa, ikionesha fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo, mahitaji ya uwekezaji katika fursa hizo, hatua kadhaa za kufuata, matarajio mbalimbali, kiwango cha nguvu kazi inayopatikana, miundombinu, taratibu za umiliki ardhi, masoko, huduma mbalimbali zilizopo katika maeneo ya uwekezaji n.k.

Kuhusu Mradi wa Ufugaji kuku Mbande, imeelezwa kwamba ni miongoni mwa miradi inayofadhiliwa na LIC katika Wilaya ya Kongwa; Wazo la mradi lilitokea katika Idara ya Mifugo na Uvuvi. Mradi huu upo katika mfumo wa kongano (Cluster) ambapo wadau mbalimbali wanahusika katika utekelezaji wa mradi huu. Wadau wanaohusika katika kutekeleza mradi huu ni pamoja na wafugaji wa kuku, wauzaji wa pembejeo zinazotumika katika ufugaji wa kuku kama vile vyakula, vyombo vya chakula na maji, wauza madawa na wauza vifaranga. Mradi huu utatekelezwa katika kipindi cha miaka mitano kwa awamu kuanzia Julai 2017.

Aidha, Kikao hicho cha pamoja kimetoka na maazimio mbalimbali katika kufanya Baraza la Biashara la Wilaya kuwa endelevu pamoja na uboreshaji wa mazingira ya kiuwekezaji wilayani Kongwa; Makubaliano haya ni:-

  • Afisa Biashara (W) aandae bajeti ya Tamasha la kutangaza fursa za uwekezaji na aiwasilishe kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Kongwa;
  • Uitishwe utaratibu ambao utafanya kila Kata ipate fursa ya kujitangaza katika tamasha la uwekezaji litakaloandaliwa;
  • Vitafutwe vyanzo madhubuti vya mapato kupata fedha za kuendesha shughuli za Baraza la Biashara baada ya kikomo cha uwekezaji wa ufadhili wa Local Investment Climate ( LIC);
  • Taarifa na mochoro ya maeneo ya uwekezaji yatakayokwa yameainishwa iwasilishwe katika kikao cha Baraza la Madiwani cha mwezi Januari 2018;
  • Kiundwe Kikosi Kazi (Task force) ya kuandaa Dira ya Uwekezaji (Investment Guide) ambayo itatumiwa kama muongozo wa Wawekezaji Wilayani Kongwa.

Maelezo ya Mradi wa Ufugaji Kuku(Namna utekelezaji unavyofanyika na jisniz ya wananchi kujiunga na mradi huu).doc

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.