• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

KONGWA YAPUNGUZA IDADI WASIOJUA KUSOMA KUANDIKA NA KUHESABU

Imewekwa: August 15th, 2025

KONGWA YAPUNGUZA IDADI YA WASIOJUA KUSOMA KUANDIKA NA KUHESABU

Na Bernadetha Mwakilabi

Habari -Kongwa DC

Idara ya Elimu Msingi Kitengo cha Elimu Watu Wazima Wilaya ya Kongwa imepongezwa kwa kupunguza idadi ya watu wazima wasiojua kusoma kuhesabu na kuandika kwa 30% ikiwa imepungua kwa 8.3% kwa takwimu ya sensa ya mwaka 2012 ambapo ilikuwa na 38.3%.

Pongezi hizo zimetolewa jana na Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Kongwa Bw Sudi Abdul alipokuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya juma la elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi yaliyokuwa na kaulimbiu “kukuza kisomo katika zama za kidigitali kwa maendeleo endelevu ya Taifa letu” yaliyofanyika kiwilaya katika kata ya hogoro ambapo ameeleza kuwa kwa karne hii ya sayansi na teknolojia ni aibu mtu mzima kutokujua kusoma kuandika na kuhesabu.

Mgeni Rasmi, Afisa elimu Sekondari Wilaya ya Kongwa Bw. Sudy Abdul akiongea na Wananchi wa Kata ya Hogoro

Bw Abdul amefafanua kuwa elimu ya watu wazima sio kujua kusoma kuandika na kuhesabu tu lakini ni pamoja na kupata stadi mbalimbali za Maisha ili kupata maendeleo kama vile stadi za kilimo, ushonaji, na biashara.

Aidha bw Abdul ametoa wito kwa wazazi kuhakikisha wanawapeleka shule Watoto wote waliopo nyumbani kwani bado kuna wimbi kubwa la watoto wasiosoma ili kurahisisha utekezaji wa program ya Mpango wa Elimu kwa Watoto Waliokosa (MEMKWA).

Baadhi ya Wananchi wa Kata ya Hogoro walioshiriki katika maadhimisho hayo

Akiongea kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Kongwa Afisa Elimu Sekondari Bi Magreth Temu amewataka Wananchi kukitumia kituo cha Elimu ya Watu Wazima kilichopo Kata ya Hogoro kupata elimu na ujuzi wanaouhitaji ili kuwasaidia kupata kipato cha familia zao.

Bi Margreth Temu Afisa Elimu Msingi Wilaya ya Kongwa  akiongea na Wananchi kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji.

Pia bi Temu amehimiza jamii kutumia fursa za maendeleo ya kiteknolojia kupata mawasiliano na kukuza uchumi na sio kutuma matusi na mambo yasiyofaa.

Pamoja na hayo nae Bi Jane Lutego Afisa Elimu watu wazima Wilaya ametaja changamoto zinazokabili utekelezaji wa elimu watu wazima kuwa ni pamoja na mwitikio hafifu wajamii, kutoungana kwa wataalam wanaoshughulikia elimu hiyo na uwezeshaji hafifu wa shughuli za elimu ya watu wazima.

Afisa elimu watu wazima Wilaya akisoma taarifa mbele ya mgeni rasmi.


Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kazini September 23, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili September 02, 2025
  • Tangazo la nafasi ya kazi June 13, 2025
  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • JAMII IMETAKIWA KUTAMBUA HAZI ZA MNYAMAKAZI PUNDA

    September 26, 2025
  • RC SENYAMULE AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MADARASA SHULE YA MSINGI KONGWA

    September 25, 2025
  • KITUO CHA AFYA KUJENGWA KATA YA SAGARA

    September 22, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII AJIRA MPYA WALA KIAPO

    September 19, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.