• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Kongwa Yatia Fora kwa Miradi Mbio za Mwenge wa Uhuru

Imewekwa: July 31st, 2018

Jumla ya miradi minne (4) yenye thamani ya Tsh. 1,744,901,951/= imepitiwa na Mwenge wa Uhuru ambapo Halmashauri ya Wilaya imechangia Tsh. 68,992,500/=, Wahisani Tsh. 371,737,200/=,

Serikali Kuu Tsh. 1,225,552,251/=, Sekta binafsi 70,000,000/= na Wananchi Tsh. 8,620,000/= .

Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018 Wilayani Kongwa umefanya shughuli zifuatazo; Kuweka jiwe la Msingi Ujenzi wa miundombinu katika kituo cha Afya Mlali; Kuzindua Ujenzi   wa Madarasa katika    Shule ya   Sekondari Laikala; Kufungua Mradi wa Maji katika Kijiji cha Machenje; Kuweka  Jiwe la Msingi Ujenzi  wa Kituo cha Kongano la Biashara ya Kuku wa Asili.

Mradi wa Kituo cha Afya Mlali:

Imeelezwa kwamba mradi hadi kufikia siku ya kupitiwa na Mwenge wa Uhuru umekamilika kwa asilimia 95 ambapo jumla ya majengo matano (5) yamejengwa. Majengo hayo ni Nyumba ya Mtumishi, Jengo la kuhifadhi Maiti, Jengo la Maabara, Jengo la Wodi ya Akina Mama na Jengo la huduma ya Upasuaji. Mradi huu umegharimu   kiasi cha Tsh.408,216,000/= kati ya fedha hizi; Tsh.400,000,000/=  zimetolewa  na  Serikali,  Tsh.4,596,000/= zimetolewa  na Halmashauri ya Wilaya na zilitumika kwa ajili ya shughuli mbali mbali za usimamizi wa ujenzi wa Majengo. Wananchi wamechangia Tsh.3,620,000/= kwa kutoa nguvu zao

kwa kufanya usafi katika eneo la kituo pamoja na kufanya usimamizi kupitia Kamati za Ujenzi, Manunuzi na Mapokezi. Mradi huu utaboresha mazingira ya kutolea huduma za Afya na pia utasaidia kuboresha makazi ya watumishi. Aidha mradi huu utasaidia kupunguza vifo vya akina mama vitokanavyo na uzazi.

Mradi wa Ujenzi wa Madarasa Shule ya Sekondari Laikala:

Mradi umetekelezwa na Halmashauri kwa Kushirikiana na Ofisi ya Rais – TAMISEMI pamoja na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Programu ya Lipa Kulingana na Matokeo (P4R). Lengo la Mradi huu ni kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia ikiwa ni utekelezaji wa sera ya Elimu bila malipo. Miundombinu hii inatoa fursa kwa wanafunzi kujifunza katika mazingira rafiki na wezeshi. Mradi huu umekamilika na umegharimu jumla ya shilingi 86,600,000, kati ya fedha hizi Tsh. 80,000,000/= zimetumika kujenga vyumba vya madarasa 4 na viti/meza 160 na Tsh. 6,600,000/= zimetumika kujenga matundu 6 ya vyoo.

Mradi wa Maji katika Kijiji cha Machenje:

Mradi ulianza tarehe  07/07/2017 na umekamilika tarehe 30/06/2018, Mradi umejengwa na Mkandarasi   NOLC ENGINNERING CO. LTD ukiwa na lengo kuu la mradi ni kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi wa Kijiji cha Machenje kutoka 21% Mwaka 2015/2016 hadi 100% Mwaka 2017/2018. Gharama za Mradi huu ni Tsh. 743,952,251/= kwa mchanganuo ufuatao; Mchango wa Serikali Kuu na Wahisani wa Maendeleo 738,952,251/=; Wananchi 5,000,000/=.

Mradi wa Kongano la Biashara ya kuku wa Asili Wilaya ya Kongwa:

Wazo la mradi lilitokea katika Idara ya Mifugo na Uvuvi baada ya kuona changamoto katika masoko ya kuku wa  asili.  Mradi  huu  upo  katika  mfumo  wa  kongano  (Cluster)  ambapo  wadau mbalimbali wanahusika katika utekelezaji wa mradi. Wadau wanaohusika katika kutekeleza mradi huu ni pamoja na wafugaji wa kuku, wauzaji wa pembejeo zinazotumika katika ufugaji wa kuku kama vile vyakula, vyombo vya chakula na maji, wauza  madawa  na  wauza  vifaranga.  Mradi  utaanza  kutekelezwa  katika  kata  tano ambazo ni Kongwa, Sejeli, Mkoka, Mtanana na Kibaigwa. Wafugaji kutoka katika kata zingine wataongezwa kadiri utekelezaji utakavyokuwa ukiendelea.

Lengo la mradi ni kuboresha kipato cha Mwananchi mmoja mmoja na Halmashauri kwa ujumla kwa kuwaunganisha   wafugaji wa kuku wa asili kwa pamoja ili kupata soko la kuku na mazao yake.

Mradi hadi utakapokamilika unatarajiwa kugharimu Tsh. 506,133,700/=, kati ya hizo; Tsh 70,000,000/= tunatarajia kukopa benki, Halmashauri itachangia Tsh 64,396,500/= na Wahisani Serikali ya Denmark kupitia mradi wa Local Investment Climate (LIC) wanatarajia kuchangia Tsh. 371,737,200/=. Hadi sasa jumla ya Tsh. 243,362,500/= zimeshapatikana kutoka LIC na jumla ya Tsh. 168,136,999/= zimeshatumika.  

Aidha, katika miradinyote iliyopitiwa na Mbio hizi za Mwenge wa Uhuru hakuna mradi uliotolewa kasoro au dosari na kukatliwa na Kiongozi Mkuu wa Mbio hizo Mhe Harles Francis Kabeho.

Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2018 umebeba Ujumbe unaosema; Elimu ni Ufunguo wa Maisha; Wekeza sasa kwa Maendeleo ya Taifa letu”. Sanjari na ujumbe huu ni, Tuwasikilize na kuwashauri Watoto ili wasitumie Dawa za kulevya, mapambano dhidi ya Rushwa “Kataa Rushwa- Jenga Tanzania” mapambano dhidi ya Ukimwi “Mwananchi Jitambue pima Afya yako sasa” na mapambano dhidi ya Malaria “Shiriki kutokomeza Malaria”.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.