Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WATAKIWA KUDHIBITI MIANYA YA RUSHWA.

Imewekwa: October 18th, 2024


"Kila mmoja wetu akitimiza majukumu yake kwa kufuata Sheria na taratibu, Serikali haitapoteza fedha kutokana na vikundi kushindwa kulipa mikopo."

Hayo yameelezwa Oktoba 29 2024 na Mkuu wa TAKUKURU wilaya ya Kongwa Bw Cosmas Shauri wakati akitoa semina kwa maafisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya ya Kongwa kuhusu kupambana na kuzuia mianya ya Rushwa katika mchakato wa utoaji wa mikopo 10% kwa vikundi vya wanawake vijana na watu wenye ulemavu.



Bwana Shauri amesema utoaji mikopo wa awali haukuwa mzuri sana na kupelekea hadi sasa vikundi vingi bado vinadaiwa hivyo taasisi imeona ni vema kutoa elimu hii ili kusaidia maafisa hao kutambua na kusimamia vema majukumu yao ili kufanikisha kupata vikundi vyenye sifa ya kukopa na kurejesha mikopo kwa wakati na kuiepushia serikali hasara.

Kwa upande wake Bw Peter Makwaya kutoka Kata ya Hogoro amesema semina hiyo itamsaidia katika kazi yake ya kutoa mikopo, kutambua kuwa kuzuia na kupambana na rushwa si kazi ya TAKUKURU bali ni jukumu la kila mwanajamii, pia wananchi wanatakiwa wafahamu kuwa kupata mikopo ni haki yao bila kutoa fedha wala zawadi yoyote kwa maafisa Maendeleo ya Jamii au kiongozi yeyote ili wapate mikopo hiyo.

Nae Bi Betha Mwanitu amesema amejifunza mambo mengi kuhusiana na rushwa katika kazi yake ya kushughulikia vikundi vinavyohitaji mikopo kwamba katika majukumu ya kila siku mwananchi anaweza kutengeneza mazingira ya kutoa rushwa Kwa kukupa zawadi ili umfanyie jambo fulani, au mwananchi anaweza kumfata kiongozi nje ya muda wa kazi ili kuomba huduma fulani kwa upendeleo ambapo anaweza kutengeneza mazingira ya rushwa.

Bi Betha ameweka wazi kuwa semina hiyo ni muhimu sana kwao na pia maafisa Maendeleo ya Jamii wataepukana na mazingira yote yanayoweza kujitokeza yanayoaashiria utoaji au upokeaji wa rushwa kwani ni wajibu wao kama viongozi kuwahudumia wananchi wote lakini ni lazima wawe makini na kufanya kazi kwa uadilifu bila kumpendelea mtu yeyote.

Semina hiyo iliyofanywa na ofisi ya TAKUKURU wilaya ya Kongwa ni mwendelezo wa semina nyingi zinazofanywa kwa makundi mbalimbali yakiwemo kama maafisa wa polisi, viongozi wa dini na Sasa maafisa Maendeleo ya Jamii lengo likiwa ni kudhibiti mianya ya Rushwa katika jamii hususani katika kipindi hiki cha uchaguzi.

Matangazo

  • Tangazo la nafasi ya kazi June 13, 2025
  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.