• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Mabaraza ya Migogoro yatakiwa kutoa haki kwa Wananchi

Imewekwa: May 23rd, 2024

Na Stephen Jackson, Kongwa DC

Mbunge wa Jimbo la Kongwa na Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai ameyataka Mabaraza ya Migogoro Wilayani Kongwa kutoa haki kwa Wananchi ili kudumisha amani katika maeneo yao.

Mhe. Ndugai amesema hayo Mei 23, 2024 katika kikao cha Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango wakati wa kujadili agenda ya yatokanayo na kikao kilichopita, ambapo iliazimiwa Mabaraza yote yaliyokosa sifa kwa kumaliza muda wake yahuishwe.

Mhe. Ndugai ametoa wito kwa wajumbe wa Mabaraza hayo kuhakikisha wanazingatia misingi ya haki wakati wa maamuzi yao, badala ya kuwa kikwazo cha upatikanaji wa haki.

Kuhusu ustawi wa watumishi, Mhe. Ndugai ameshauri watumishi kujiunga kwenye vyama vya ushirika vya kuweka na kukopa SACCOS ili kupunguza changamoto za kiuchumi baina yao.

Akifafanua hoja hiyo, Mkuu wa Kitengo cha huduma za Kisheria Wakili Hella Mlimanazi alisema, mchakato huo unaendelea chini ya Kamati za maendeleo za Kata, ambapo jumla ya Mabaraza 13 yaliyomaliza muda wake yanatarajiwa kuhuishwa chini ya maelekezo ya Halmashauri katika kipindi cha siku kumi na nne (14) kuanzia Mei 21, 2024.

Kwa mujibu wa Maelekezo, Mabaraza hayo hushugulikia migogoro ya Ardhi, familia na jinai ndogo ndogo kwa lengo la kukuza dhana ya usuluhishi baina ya Wananchi.

Akijibu hoja ya Mkaguzi wa ndani bwana Jacob Mgusi iliyojikita kwenye uhafifu wa marejesho ya mikopo ya Asilimia 10% iliyotolewa kupitia Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Jinsia wanawake na Makundi Maalumu, Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Jinsia, wanawake na Makundi Maalumu Bi. Paskalina Duwe amesema takribani shilingi milioni 482 zinadaiwa kutoka kwa vikundi, hivyo ameiomba Menejimenti kutatua changamoto ya usafiri ili kuongeza kasi ya ufuatiliaji.

Akihitimisha kikao hicho Mhe. White Zuberi Mwanzalila Mwenyekiti wa Halmashauri,  amewataka Wakuu wa Divisheni na Vitengo kuhakikisha wanasimamia kikamilifu matumizi ya fedha zinazotolewa na Serikali, ikiwa ni pamoja na fedha za ujenzi wa Jengo jipya la Halmashauri.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.