• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Mamia Wamuaga Marehemu Sarah Lujeli Aliyekuwa Diwani Viti Maalumu

Imewekwa: August 4th, 2021

Na Stephen Jackson, Kongwa

Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali akiwemo Mkuu wa wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius Mwema Emmanuel, wamehudhuria Ibada ya mazishi ya aliyekuwa Diwani wa Viti maalumu kata ya Matongoro, Marehemu Sarah Elia Lujeli ambaye amefariki dunia tarehe 2 Agosti 2021 katika Hospitali ya Rufaa Mbeya.

Akizungumza na waombolezaji, Mhe. Mwema amewasisitiza waombolezaji kutambua thamani ya uhai wao na kuujali, hivyo wanao wajibu wa kuchukua Tahadhali dhidi ya ugonjwa hatari wa ‘’corona’’ na ameahidi kupata chanjo ya ugonjwa huo ambayo Kiwilaya ilipangwa kuzinduliwa tarehe 5 Agost 2021.

Kufuatia msiba huo, Salamu mbalimbali za rambirambi kutoka kwa viongozi wa Chama Tawala CCM, Halmashauri ya Kongwa na Makundi mbalimbali ya Kijamii zimetolewa.

Akiwasilisha salamu hizo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya, Afisa Tawala Ndugu Geofrey Mville alisema, Marehemu Sarah Elia Lujeli alizaliwa Tarehe 30 Desemba 1966 katika Kijiji cha Matongoro na alijiunga na duru za kisiasa tangu mwaka 1994  na kufanikiwa kushika wadhifa wa Diwani viti Maalumu pamoja na nyadhifa nyingine kwa nyakati tofauti hadi alipofikwa na umauti.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kongwa White Zuberi Mwanzalila pamoja na kutoa salamu za pole kwa waombolezaji wote pia amemshukuru Mbunge wa Jimbo la Lupa Kutoka Chunya Mbeya, Chief Masache Njelu Kasaka kwa jitihada za kuusafirisha mwili wa Marehemu Sarah kutoka mkoani Mbeya hadi kufikishwa nyumbani kwake Matongoro.

Kuhusu ugonjwa wa Covid 19 Mhe. White Zuberi Mwanzalila amewataka wananchi kuendelea kuchukua Tahadhari kwa kunawa mikono na kutumia vitakasa mikono pia kupata chanjo ambayo imeanza kutolewa. "Na bahati nzuri zimeshaletwa chanjo. Chanjo ziko, tutakuwa na vituo vyetu vya Afya vitatoa huduma ya chanjo kwa yule anayetaka, na naamini baada ya muda mfupi, kila mmoja atachanja" Amesema White Zuberi Mwanzalila.

Akizungumza Kwa niaba ya Mbunge wa Jimbo la Kongwa, Mbunge wa Jimbo la Lupa Chief Kasaka, amewataka wananchi kudumisha mazuri yote aliyoyafanya Marehemu Sarah kipindi cha Uhai wake Kama ishara ya kumkumbuka.

Aidha viongozi wengine wa CCM waliopata fursa ya kutoa salamu zao za rambirambi ni pamoja na Mhe. Pili Mbanga Katibu CCM Mkoa, Ferister Bura Mbunge Mstaafu viti maalumu Mkoa, Marco Mbanga Katibu CCM Wilaya ya Kongwa, Henry Msunga, Katibu Mwenezi CCM mkoa, na Mariam Kret Katibu UWT Mkoa.

 Ibada ya mazishi ya Marehemu Sarah Elia Lujeli imeongozwa na Canon Jackson Lwanda wa kanisa la Anglikana Parishi ya Mkoka, na kuhudhuriwa na mamia ya waombolezaji wakiwemo viongozi wa CCM ngazi ya Mkoa, wilaya, kata na kijiji, Uongozi wa Halmashauri, Madiwani na wananchi

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.