• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Marufuku Utupaji wa Taka Ovyo Eneo la Hifadhi ya Ranchi ya Taifa NARCO

Imewekwa: June 5th, 2018

Katibu Tawala Wilayani Kongwa Bw. Audiphace Mushi akimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, amepiga marufuku Utupaji wa Taka ovyo, kwa Wananchi na wageni wapitao Katika eneo la Hifadhi ya Ranchi ya Taifa (NARCO) iliyopo wilayani humo na kuwa na desturi ya utunzaji wa Mazingira ili kuepuka uchafuzi holela wa Mazingira.

Akizungumza na wafanyabiashara ndogondogo wa barabarani na wafanyakazi wa NARCO katika kituo cha mabasi cha Njia Panda ya Kiteto kilichopo eneo la NARCO katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani amesema, ni muhimu kufanyia usafi eneo hilo kila siku, na kuwa walinzi wa watupa taka wakiwemo abiria wa magari mbalimbali yanayosimama kwa ajili ya kununua bidhaa zao.

Aidha, amewataka Wananchi hao kutambua ya kuwa kuharibu Mazingira kunagharimu vizazi na vizazi, kutokana kutumia muda mrefu kutunza miti na uoto wa asili lakini katika kukata miti au kuchoma moto uoto wa asili hutumia sekunde chache.

Ambapo Sherehe hizo zilipambwa Kauli mbiu Kitaifa ilikuwa "Mkaa ni Gharama Tumia Nishati Mbadala"

Mushi alisema kimsingi vitendo vya Kibinadamu ndio Chanzo cha Uharibifu wa Mazingira, ikiwa ni pamoja na uchimbaji holela wa madini, ukataji miti ovyo, urinaji wa asali kwa kuchoma moto, uvamizi wa shughuli za kilimo maeneo ya milima.

Kadhalika alieleza kuwa, upo uchafuzi wa Taka ngumu eneo la Hifadhi ya NARCO, kama mifuko ya plastiki, makopo ya plastiki ambazo hutupwa na mabasi ya abiria na magari ya mizigo, pamoja na makondakta kutapisha vyombo vyao vya uchafu ndani ya Hifadhi. "Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya itakaa hivi karibuni na itatoa Tamko dhidi ya wachafuzi Mazingira NARCO", amesisitiza.

Meneja NARCO Kongwa Bw. Euzebius Mutayabarwa alisema watamchulia hatua Kali za kisheria mtu yoyote watakaembaini anakata miti Katika Ranch hiyo bila kibali, pamoja na watakaovamia eneo hilo kwa ajili ya kilimo, na atakayechoma nyasi za moto kwenye eneo hilo, kwani ni malisho ya mifugo iliyopo katika Ranchi hiyo.

Aidha, ametoa ahadi ya kujenga choo katika kituo hicho ili kuepusha abiria wanachimbao dawa ovyo katika eneo hilo, na kuwataka vijana wafanyao biashara ndogondogo kujisajili na kutambulika na kuwa walinzi dhidi ya watupa taka na kukitunza na kukisimamia choo hicho.

Naye Kaimu Afisa Mazingira (W) Wilayani Kongwa, Bw. Godfrey Mujairi amesema kauli mbiu ya Mhe. Rais wa Awamu ya Tano Dkt. John Magufuli, inahamasisha Viwanda, hivyo viwanda haviwezi kuwepo kama uharibifu wa Mazingira, kwani malighafi na nishati, vyote hutokana na mazingira.

Mujairi ameongeza kuwa Utunzaji wa Mazingira usiishie siku ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Bali iwe ni Desturi yao Kila Siku kabla ya kufungua biashara.


Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.