• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Yafurahia Kikao cha DC

Imewekwa: August 30th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe Remidius Mwema Emmanuel ameendesha Kikao maalum na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGOs) yanayofanya kazi ndani ya Wilaya ya Kongwa chenye lengo kuu la kuweza kufahamiana wadau kwa wadau na Uongozi wa Wilaya ya Kongwa, kupata taarifa za kazi tangu utekelezaji wa mradi hadi wakati huu na Uongozi kuweza kutambua shughuli za wadau kwa kila eneo.

Mkutano huu umefanyika leo tarehe 30 Agosti, katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa ambapo jumla ya NGOs 16 zilishiriki na kutoa taarifa zao kuhusu shughuli mbalimbali wanazozifanya Wilayani Kongwa, changamoto wanazokumbana nazo, pamoja na kutoa maoni yao kwa uongozi wa Wilaya ya Kongwa kuhusu maendeleo ya Kongwa. Baadhi ya NGOs zilizoshiriki ni World Vision, TAYOA, TIST, KTP, TAFARMO, UFUNDIKO, Nurture Tanzania, ERGPAF, Compassion, BRAC, CCT Mwanamke Jasiri, LYVIA, CIS, Rafiki Dodoma na Wildaf.  

Mhe Remedius ametoa maelekezo kwa NGOs zote kutoa taarifa zinazoendana na uhalisia na kutoa ushirikiano kwa Idara ya Maendeleo ya Jamii inayosimamia NGOs zote na idara zingine ambazo zinahusiana moja kwa moja na miradi inayofanyika ili miradi ifanyike katika maeneo yenye mahitaji zaidi.

Mhe Remidius pia, amezihakikishia NGOs zote kwamba, kila NGO inavyofanya kazi Wilayani Kongwa ataitembelea kuona shughuli zake katika maeneo husika na atatoa vyeti vya utambuzi kwa kila NGO kutambua mchango wake katika maendeleo ya Wilaya ya Kongwa.

“NGO yeyote inapopata changamoto katika maeneo inapofanyakazi isisite kuwasiliana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Wilaya yupo ili kusaidia utatuzi wa changamoto mbalimbali”, amesema Mhe Remidius.

Mhe Remidius ameagiza NGOs zote ambazo hazikufika katika Kikao bila taarifa ziandikiwe barua kwani zinachafua NGOs zingine zinazofanya kazi vizuri katika Wilaya ya Kongwa na Idara ya Maendeleo ya Jamii kuandaa fomati ya taarifa ambayo kila Shirika lisilo la Kiserikali (NGO) itaitumia katika kuwasilisha taarifa zake Wilayani na NGOs hizo zikajipange na kuwasilisha taarifa rasmi kabla ya tarehe 10 Septemba 2021.

NGOs zilizoshiriki zimefurahi sana kwani hawakuwahi kukutana na wengi walikuwa hawafahamiani, hivyo, kikao hiki kimekuwa jukwaa zuri kwao kwa kuweza kufahamiana na kumuomba Mhe Mkuu wa Wilaya kufanya vikao hivi kila baada ya miezi 3, ambapo ombi lao limeridhiwa.

Naye Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Bibi Paskalina T. Duwe akimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji Wilaya amesema vikao vya kukutana na NGOs ni vya kisheria na Idara yake imejipanga katika kuhakikisha vikao kama hiki vinafanyika kila baada ya miezi 3 na kuziomba NGOs kutoa ushirikiano kwa baadhi ya mambo yatakayo hitajika kutoka kwao kwa maandalizi ya vikao.

Mwisho, Mhe Remidius amezikaribisha NGOs zote kushiriki Kongamano la Maendeleo ya Wilaya ya Kongwa litakalofanyika tarehe 11 Septemba, 2021 katika Ukumbi wa VETA Kongwa ambapo Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Kongwa Mhe Job Ndugai, Viongozi wote wa Wilaya, Waheshimiwa Madiwani wa Kongwa, wenyeviti wa vijiji na vitongoji na wadau mbalimbali wa maendeleo ya Kongwa watakuwepo.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.