• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Ahoji sababu za baadhi ya Walimu kutopandishwa Madaraja

Imewekwa: October 16th, 2022

Na Stephen Jackson, Kongwa

Mbunge wa Jimbo la Kongwa na Spika mstaafu wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai amewataka viongozi wanaoshughulikia maslahi ya walimu ikiwemo upandaji wa Madaraja kuhakikisha wanatekeleza wajibu wao kikamilifu Ili kuharakisha upatikanaji wa haki za walimu.

Mhe. Ndugai, ameeleza hayo wakati  alipokuwa akihutubia Mkutano mkuu wa nusu muhula wa chama cha Walimu Tanzania (CWT) Wilaya ya Kongwa,  uliofanyika Jumamosi ya Tarehe 15 Oktoba, 2022 katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Kongwa.

Ameongeza kuwa kupitia dhamana aliyonayo kama mwakilishi wa wananchi, ataendelea kushirikiana na CWT katika kufanikisha upatikanaji wa haki za walimu hususani upandaji wa Madaraja.

Naye Mwenyekiti wa chama cha Walimu Tanzania (CWT) Wilaya ya Kongwa Mwalimu Majuto Deus, pamoja na kumshukuru Mhe. Mbunge kwa kukubali kuwa mgeni rasmi katika Mkutano huo,  pia ameahidi kuwa CWT itahakikisha walimu wanatimiza wajibu wao wa kuwafundisha wanafunzi na hatinaye kuinua ufaulu wa wanafunzi Wilayani Kongwa.

Kwa upande mwingine Mhe. Ndugai amewashauri wasimamizi wa  shughuli za elimu kutoa fursa zinazopatikana  kwa kuzingatia misingi ya usawa.

Kufuatia Ushauri huo, Afisa Elimu Msingi Bwn. Eugine Shirima, amekiri kuwepo kwa changamoto ya kujiridia rudia kwa wasimamizi wa mitihani hasa ya elimu ya msingi kutokana na sheria ya mitihani ambayo inawataka walimu wa shule za sekondari kusimamia mitihani ya shule za msingi, huku idadi yao Ikiwa ni ndogo ikilinganishwa na Idadi ya mikondo ya wanafunzi.

Naye Mwenyekiti wa CWT Mkoa wa Dodoma Mwalimu Samwel Malechela, amempongeza Mhe. Job Ndugai kwa usimamizi mzuri wa miradi ya Maendeleo katika Jimbo la Kongwa hasa ujenzi wa miundombinu, zikiwemo barabara na Madarasa ya kisasa.

Nao wajumbe mbalimbali wa Mkutano wamewataka viongozi wa CWT kulinda na kusimamia vema mali za chama, na kufuatilia haki zao katika mifuko ya hifadhi ya jamii, bima ya Afya pamoja na taasisi za kiuchumi zinazohudumia walimu ikiwemo Benki ya Mwalimu.

Katika hatua nyingine Mkutano huo umepitisha azimio la kununua gari aina ya "Coaster" kwa ajili ya kutatua changamoto ya usafiri kwa wanachama kipindi wanapolazimika kusafiri kama chama kushiriki misiba na hafla mbalimbali huku chanzo Cha Fedha kikitajwa kuwa ni marejesho ya wanachama.

Mkutano huo umehusisha viongozi wa CWT ngazi ya Mkoa, Wilaya, uwakilishi mahala pa kazi pamoja na baadhi ya wadau wake ambao ni viongozi kutoka Halmashauri na Tume ya Utumishi wa walimu (TSC)



Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.