• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Mhe. Majaliwa ataka Miundombinu Rafiki kwa wajasiriamali Kituo Atamizi cha Ufugaji wa kibiashara kwa Vijana-Mbande.

Imewekwa: May 13th, 2024

Na Stephen Jackson, Kongwa.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwaa meitaka Taliri na Wizara ya Mifugo kuweka mazingira rafiki katika Kituo Atamizi cha Ufugaji wa kibiashara kwa Vijana kilichopo eneo la Mbande Kata ya Sejeli ili kuwezesha Vijana wengi kufanya biashara ikiwemo nyama choma.

Mhe. Majaliwa amesema Wizara ya Mifugo na uvuvi, Taliri kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa ni vema wakaweka Miundombinu itakayowawezesha Vijana wanaojihusisha na shughuli za ujasiriamali kupitia uchomaji nyama Kijiji cha Mbande na maeneo mengine  kuhamishia shughuli zao katika Kituo cha Taliri Kilichopo eneo la Mbande Kata ya Sejeli.

Mhe. Majaliwa alisema hayo wakati akihutubia Wananchi kwenye hafla ya makabidhiano ya Kituo Atamizi cha Ufugaji wa kibiashara kwa Vijana - Kongwa kati ya "Private Agricultural Sector Support" (PASS) na Kituo cha utafiti wa mifugo Taliri.

Mhe. Majaliwa alisisitiza Wizara ya Mifugo na uvuvi kufanya kazi kwa ukaribu na uongozi wa Halmashauri ili kukuza ufanisi wa Kituo hicho kwani Wakuu wa Divisheni na Vitengo hususani Seksheni ya Mifugo na maendeleo ya Jamii kwa ajili ya ushauri wa kitaalamu.

Mhe. Majaliwa alitutumia fursa hiyo kuhamasisha Wananchi kujitokeza kwa wingi katika kwenye maboresho ya daftari la kudumu la wapiga kura sanjari na kushiriki kutoa maoni yao katika maandalizi ya dira ya maendeleo ya taifa 2050.

Akihitimisha hotuba yake Mhe. Majaliwa, aliipongeza Wizara ya Mifugo na uvuvi, PASS na Taliri kwa kufanikisha kukamilika kwa Kituo hicho.

Kwa upande wake Mhe. Abdala Ulega, Waziri wa Mifugo na Uvuvi aliutaarifu umma kuwa nyama ya mbuzi inapendwa kwa asilimia 70% ikilinganishwa na nyama nyingine huku nyingi ikitoka mkoani Dodoma.

"Nyama ya mbuzi inayoongoza kwa kuoendwa ni Ile inayotoka katika mkoa wa Dodoma" 

"Kituo kikubwa cha nyama ya mbuzi hapa nchini kitakuwa ni hapa Kongwa" Abdallah Ulega Waziri wa mifugo na uvuvi.

Katika Hafla hiyo viongozi mbalimbali walizungumza na Wananchi akiwemo Mhe. Rosemary Senyamule Mkuu wa Mkoa wa Dodoma

ambaye alisema katika kipindi cha miaka mitatu Mkoa wa Dodoma umepata miradi mikubwa kama vile ujenzi wa majosho 59, mizani 13 inayotumika minadani, ukarabati wa machinjio manne, minada miwili imewekwa uzio, pikipiki 45 za wataalamu wa mifugo, dawa za kuogeshea mifugo, Mifugo 332,000 ilipatiwa chanjo, ujenzi wa malambo manne ya maji na ujenzi wa mabwawa mawili katika Wilaya za Kongwa na Chamwino unaendelea. Aidha Senyamule ameeleza kuwa Mkoa umefanikiwa kutatua baadhi ya migogoro ya wakulima na wafugaji ilitodumu kwa muda mrefu.

 Mhe. Job Ndugai Spika Mstaafu na mbunge wa Jimbo la Kongwa aliyeshauri Vijana waanzilishi wa Kituo hicho cha unenepeshaji mbuzi wapewe Mbuzi kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi kupitia Ufugaji waliokifunza kupitia Kituo hicho, Jambo lililoungwa mkono na Waziri wa mifugo kwamba Jumla ya mbuzi 60 watatolewa kwa Vijana hao.

Akizungumza kwa niaba ya bodi ya wakurugenzi wa PASS, Bwana  Charse Chenza Mwenyekiti wa bodi hiyo alisema, Pamoja na mambo mengine,  PASS ipo kuwezesha Wananchi, vikundi  makampuni au wakulima wasio na dhamana ya kukopesheka benki, hivyo jukumu la PASS ni kuwawekea dhamana.


Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.