• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Mkurugenzi Kongwa apongezwa kwa Uadilifu

Imewekwa: November 3rd, 2021

Na Stephen Jackson, Kongwa.

Baraza la Madiwani katika Halmashauri ya wilaya ya Kongwa kupitia Mwenyekiti wake Mhe. White Zuberi Mwanzalila, limempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Dkt. Omary Nkullo Kutokana na utendaji wake wa kazi unaozingatia nidhamu ya Matumizi ya Fedha za wananchi.

Mheshimiwa Mwanzalila ametoa pongezi hizo wakati akihitimisha Mkutano wa Baraza la Madiwani tarehe 03 Novemba, 2021 lililoketi kupokea taarifa za Kamati za Kudumu na taarifa za Mamlaka za miji midogo ya Kongwa na Kibaigwa kwa kipindi cha robo ya kwanza ya Mwaka Mwaka wa Fedha 2021/2022.

Akitoa ufafanuzi Mhe. White Zuberi Mwanzalila amesema licha ya yeye mwenyewe kufanya kazi na wakurugenzi mbalimbali, Dkt. Omary Nkullo ndiye Mkurugenzi pekee ambaye hujigharamia safari zisizo za kikazi‘’. Nimefanya kazi na wakurugenzi wengi, anapokuwa na safari binafsi anajaza gari la Halmashauri mafuta linampeleka, lakini mkurugenzi wetu ya kwake binafsi anaondoka na gari yake. Ni wakurugenzi wachache mpigieni makofi’’. Amenukuliwa Mhe. Mwanzalila.

Aidha Mwenyekiti huyo wa Halmashauri ametumia fursa hiyo kuwataka viongozi wote kila mmoja kwa nafasi yake kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii na uadilifu ili kuharakisha maendeleo ya wananchi.

Kwa upande wake Dkt. Nkullo, akiwa ndiye katibu wa Baraza hilo la madiwani, amewasilisha taarifa ya Mwenyekiti ambayo inaonesha kuwa katika kipindi cha Julai-Septemba 2021, Halmashauri ilitarajia kukusanya Jumla ya TZS. 801,971,875/= na badala yake imevuka lengo kwa kukusanya TZS. 1,114,237,540.50/= Sawa na 138.9% ya lengo.

Katika baraza hilo taasisi mbalimbali zilialikwa na miongoni mwake Wakala wa Maji na usafi wa Mazingira vijijini ‘’RUWASA’’ na Wakala wa barabara mijini na vijijini ‘’TARURA’’ ziliweza kuwasilisha taarifa zao kuhusu hali halisi ya miradi inayoendelea kutekelezwa kwa bajeti ya Mwaka wa Fedha 2021/2022.

Akiwasilisha taarifa kwa niaba ya Meneja ‘’RUWASA’’, Mhandisi Mohamedi A. Ally, amezitaja changamoto zinazoikabili taasisi hiyo kuwa ni pamoja na Fedha za miradi kutotolewa kwa wakati jambo linalozorotesha kasi ya uchimbaji wa visima, uhaba wa wataalamu na ushirikiano hafifu kwa baadhi ya viongozi wa Serikali na chama ngazi ya jamii.

Naye Kaimu Meneja wa ‘’TARURA’’ mhandisi Boniface Mandi ameeleza kuwa awali mamlaka hiyo ilitengewa bajeti ndogo lakini kwa sasa imepandishwa hivyo matarajio ni kujenga barabara nyingi zaidi ya ilivyotegemewa. Ameongeza kuwa jumla ya kilometa mbili za lami zinatarajiwa kujengwa katika Mamlaka ya mji mdogo wa Kongwa na kilometa moja katika mji wa Kibaigwa ingawa amelishauri baraza hilo kuwa ujenzi wa barabara  kwa kiwango cha changalawe utahusika katika maeneo mengi ili kurahisisha shughuli za usafirishaji wilayani Kongwa.

Mkutano wa baraza la madiwani ulioketi kupokea taarifa za Kamati za Kudumu na taarifa za Mamlaka za miji midogo ya Kongwa na Kibaigwa kwa kipindi cha robo ya kwanza ya Mwaka Mwaka wa Fedha 2021/2022, umefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ukihudhuriwa na Madiwani, wakuu wa Idara naTaasisi mbalimbali pamoja na kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya iliyoongozana na Kaimu katibu Tawala wa Wilaya Ndugu Victor Ligate.


Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.